• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Complaints |
    • Gms |
Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu ya Halmashauri
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji/Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi, Maliasili na Utalii
      • Mipango, Uchumi na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Utumishi na Utawala
      • Maji
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi na Zimamoto
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA)
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • TASAF
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Fursa za Kilimo
    • Fursa za ufugaji
    • Fursa za Madini
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Huduma za Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Mheshimiwa Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokalika
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma/Vyombo Mbalimbali vya Habari
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali

BARAZA LA MADIWANI NAMTUMBO LARIDHIA JINA LA SEKONDARI YA WASICHANA MKOA WA RUVUMA KUITWA "SAMIA GIRLS SECONDARY SCHOOL"

Tarehe ya Kuweka: September 22nd, 2022

BARAZA LA MADIWANI NAMTUMBO LARIDHIA JINA LA SEKONDARI YA WASICHANA MKOA WA RUVUMA  KUITWA “SAMIA GIRLS  SECONDARY SCHOOL”


Baraza la madiwani la Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma limepitisha kwa kauli moja kuwa jina la Sekondari ya wasichana ya mkoa wa Ruvuma inayojengwa katika wilaya ya Namtumbo kuitwa  SAMIA GIRLS SECONDARY  SCHOOL.

Akiwasilisha salamu za serikali katika baraza la madiwani pamoja na mambo mengine mkuu wa wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma Dkt Julius Kenneth Ningu alimshukuru Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha  kiasi cha shilingi bilioni 3 za kujenga sekondari ya wasichana ya Mkoa wa Ruvuma katika wilaya ya Namtumbo.

Dkt Ningu aliwaambia waheshimiwa madiwani kitendo cha ujenzi wa sekondari hiyo inaipa hadhi wilaya ya Namtumbo na mkoa wa Ruvuma kwa ujumla hali inayotupasa kushukuru kama ilivyoada kushukuru kwa kufanyiwa jambo jema .

Aidha Dkt Ningu aliwaomba waheshimiwa madiwani kuridhia jina la sekondari hiyo kuitwa Samia Girls Secondary School  kama shukrani ya wananchi wa Namtumbo  kwa Mheshimiwa Raisi wa Jamhuri ya Mungano wa Tanzania  Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha hizo za kujenga sekondari ya wasichana wilayani Namtumbo.

Hata hivyo Dkt Ningu aliwaambia waheshimiwa madiwani kilio kikubwa cha wananchi katika wilaya ya Namtumbo ilikuwa bei kubwa ya mbolea  lakini wanamshukuru mheshimiwa Raisi kwa kukubali kutoa shilingi bilioni 150 kwa ajili ya kupunguza bei ya mbolea  ili kuwapunguzia wakulima bei ya mbolea.

Lakini pia Dkt Ningu aliwaagiza waheshimiwa madiwani kuhakikisha wananchi wanaoishi na silaha katika maeneo yao kuzisalimisha kwa msamaha mwisho tarehe 30 mwezi huu septemba 2022 na baada ya hapo wananchi watakao kamatwa na silaha baada ya tarehe hiyo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao alisema mkuu wa wilaya huyo.

Diwani wa viti maalumu  Zalia Banda akiongea kwa niaba ya madiwani wenzake walimshukuru Mkuu wa wilaya huyo kwa namna anavyowapa ushirikiano katika maswala ya maendelea katika wilaya hiyo na kudai kuwa madiwani wataendelea kushirikiana naye kwa hali na mali.

Zalia Banda pia aliwasilisha ombi kwa mkuu wa wilaya kupitisha barua iliyoombwa na waheshimiwa madiwani  inayowasilishwa katika ofisi ya waziri mkuu kuhusu malalamiko ya wananchi kuhusu kukithiri kwa mifugo katika Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo na kuibuka kwa migogoro ya mara kwa mara na wafugaji huku waathirika wakubwa ni wakulimwa ambapo Mkuu wa wilaya  huyo alikubali kushughulika ombi hilo.

Naye Diwani wa kata ya mkongo Daniel Nyambo kwa upande wake alipendekeza mfumo wa ukusanyaji wa mapato wa Halmashauri utenganishwe kwa madai kuwa mfumo wa ukusanyaji wa kawaida wa mapato hautiliwi maanani na badala yake kutegemea mapato yatokanayo na stakabadhi ghalani.

Nyambo alisema ni vyema mfumo wa ukusanyaji wa mapato ya kawaida mapato yake yatenganishwe na mapato yanayotokana na ushuru wa papo kwa papo kutoka uuzaji wa mazao kwa njia ya stakabadhi ghalani ili waheshimiwa madiwani wajue badala ya kuunganisha mapato yote.

Mwenyekiti wa  Halmashauri  ya wilaya ya Namtumbo  Jumma Pandu pamoja na kumshukuru mkuu wa wilaya kwa ushirikiano kati ya ofisi yake na waheshimiwa madiwani alisema madiwani wataendelea kuisimamia halmashauri na hawatasita kuchukua hatua kwa watumishi watakaoenda kinyume katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.

Shule ya sekondari ya wasichana ya mkoa wa Ruvuma  iliyopewa jina la Samia Girls Secondary School imejengwa katika kijiji cha Migelegele mamlaka ya mji mdogo wa Namtumbo ambapo Raisi wa Jamhuri wa muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan alitoa kiasi cha shilingi bilioni 3 ili kujenga majengo hayo.

NA YEREMIAS NGERANGERA

NAMTUMBO.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA 2025 KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA NAMTUMBO January 18, 2025
  • MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI KATIKA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA NAMTUMBO MWAKA 2025 January 12, 2025
  • Ona zote

Habari Mpya

  • DC NGOLLO MALENYA AWAFARIJI WAHANGA WA RADI KATIKA KATA YA LUSEWA WILAYA YA NAMTUMBO

    February 21, 2025
  • WANANCHI NAMTUMBO WAMSHUKURU RAIS SAMIA

    January 06, 2025
  • MATREKTA aliyogawa Rais Samia yawanufaisha wananchi wa Wilaya ya Namtumbo, katika kuongeza Uzalishaji kwenye kilimo cha Kisiasa.

    January 06, 2025
  • Sukrani kwa Mhe.Rais wa wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan

    January 05, 2025
  • Ona zote

Video

HOTUBA YA WAZIRI WA TAMISEMI
Video

Kurasa za Haraka

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Halmashauri ya Songea
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Nyasa
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru

Tovuti Mashuhuri

  • TAMISEMI
  • Ikulu ya Tanzania
  • Tume ya Utumishi wa Umma
  • Baraza la Mitihani
  • Tume ya ajira Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo

    Anuani: 2 Barabara ya Boma, S.L.P 55, 57382 NAMTUMBO

    Simu ya Mezani: 0252675008

    Simu ya Mkononi: 0767519181

    Barua Pepe: ded@namtumbodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki©2021Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo. Haki zote Zimehifadhiwa.