• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Complaints |
    • Gms |
Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu ya Halmashauri
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji/Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi, Maliasili na Utalii
      • Mipango, Uchumi na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Utumishi na Utawala
      • Maji
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi na Zimamoto
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA)
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • TASAF
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Fursa za Kilimo
    • Fursa za ufugaji
    • Fursa za Madini
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Huduma za Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Mheshimiwa Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokalika
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma/Vyombo Mbalimbali vya Habari
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali

MIFUGO MINGINE 508 YAKAMATWA NAMTUMBO

Tarehe ya Kuweka: January 25th, 2023

MIFUGO  MINGINE  508 YAKAMATWA  NAMTUMBO

Ng”ombe 485,Kondoo 16, Mbuzi 4 na punda 3 wamekamatwa katika kijiji cha Kitanda wilayani Namtumbo mkoani Ruvuma wakiwa hawana vibali vya kuingiza mifugo hivyo mkoa wa Ruvuma wakitokea wilaya ya Malinyi mkoa wa Morogoro.

Mtendaji wa kijiji cha Kitanda  Ayubu Muhuwa  alisema mifugo hiyo imekamatwa katika eneo la hifadhi ya msitu wa kijiji cha kitanda “Mtaungana” uliotengwa na kijiji kwa ajili ya matumizi bora ya ardhi ya kijiji hicho cha kitanda.

Muhuwa alidai mifugo iliyokamatwa katika msitu huo ni Ng”ombe 485, kondoo 16,mbuzi 4 na punda 3 wakiwa katika eneo la msitu  lililotengwa na kijiji kwa ajili ya matumizi bora ya ardhi na walipowahoji na mgambo wa kijiji hicho wafugaji hao walikiri kuwepo katika msitu huo bila vibali vyovyote na ndipo  walipoamua kuwakamata na kuwafikisha katika kituo kidogo cha polisi katika kijiji cha Kitanda .

Efrem  Mwale mwananchi wa kijiji cha kitanda alisema swala la wafugaji katika kijiji cha kitanda ni la muda mrefu kwani lilikuwa linafumbiwa macho na viongozi hali iliyowafanya wafugaji na mifugo yao kuingiza mifugo mara kwa mara kutoka Malinyi mkoa wa morogoro na kuingia mkoa wa Ruvuma kupitia kijiji cha Kitanda.

Mwale alisema anamshukuru mkuu wa mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas kwa kuanzia mpango wa kuzuia mifugo kuingia katika mkoa wa Ruvuma kwa kuwakamata wafugaji wanaoingiza mifugo mkoa wa Ruvuma bila vibali kutoka katika mamlaka husika hali ambayo inazaa matunda hisi sasa.

Aidha Mwale alidai viongozi wa vijiji walikuwa wanapigiwa kelele na wananchi kupitia mikutano ya hadhara wakilalamikia uingizaji wa wafugaji katika kijiji cha kitanda bila mafanikio kwa kile kilichoonekana kuwa baadhi ya viongozi walikuwa wananufaika na uwepo wa wafugaji hao katika maeneo ya vijiji alisema Mwale.

Afisa Mifugo wa Halmashauri ya wilaya ya  Namtumbo Paul Ambokile pamoja na kukiri kukamatwa kwa wafugaji hao amewataka  wafugaji kuzingatia taratibu ,kanuni na sheria za uingizaji au usafirishaji wa mifugo kutoka sehemu moja na kwenda sehemu nyingine kutafuta malisho.

Mifugo 508 inashikiliwa na jeshi la polisi kituo kidogo kilichopo katika kijiji cha kitanda huku utaratibu wa ulipaji wa faini ukisubiriwa na wafugaji hao kwa kosa la kuingiza mifugo katika mkoa wa Ruvuma kupitia kijiji cha kitanda wilaya ya Namtumbo na baada ya hapo utaratibu wa kurudisha mifugo hiyo ilikotoka utafanyika.

Mwisho.

Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA YA WAOMBAJI WA KAZI YA MUDA YA SENSA WALIOFAULU USAILI NA KUITWA KWENYE MAFUNZO July 27, 2022
  • TAARIFA KWA UMMA June 27, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WAOMBAJI WA KAZI YA MUDA YA SENSA WALIOFAULU USAILI NA KUITWA KWENYE MAFUNZO July 27, 2022
  • MABADILIKO YA TAREHE YA KUFANYA USAILI June 22, 2022
  • Ona zote

Habari Mpya

  • DC NAMTUMBO AWATOA HOFU WANANCHI FEDHA MILIONI 510 ZA UJENZI MRADI WA MAJI

    March 16, 2023
  • DC AAGIZA UPANDAJI NA UTUNZAJI WA MITI KWENYE CHANZO CHA MTO NAMAMBIG

    March 12, 2023
  • DC NAMTUMBO; KUKUMBATIA WAJUKUU KUJIONGEZEA UMASKINI

    March 11, 2023
  • DC NAMTUMBO AWATAKA WALIMU KUSIMAMIA MAADILI SHULENI

    March 11, 2023
  • Ona zote

Video

HOTUBA YA WAZIRI WA TAMISEMI
Video

Kurasa za Haraka

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Halmashauri ya Songea
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Nyasa
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru

Tovuti Mashuhuri

  • TAMISEMI
  • Ikulu ya Tanzania
  • Tume ya Utumishi wa Umma
  • Baraza la Mitihani
  • Tume ya ajira Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo

    Anuani: S.L.P 55 NAMTUMBO

    Simu ya Mezani: 0252675008

    Simu ya Mkononi: 0765142640

    Barua Pepe: ded@namtumbodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki©2021Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo. Haki zote Zimehifadhiwa.