• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Complaints |
    • Gms |
Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu ya Halmashauri
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji/Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi, Maliasili na Utalii
      • Mipango, Uchumi na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Utumishi na Utawala
      • Maji
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi na Zimamoto
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA)
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • TASAF
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Fursa za Kilimo
    • Fursa za ufugaji
    • Fursa za Madini
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Huduma za Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Mheshimiwa Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokalika
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma/Vyombo Mbalimbali vya Habari
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali

VGS ,MTUMISHI HALMASHAURI WAKATWA MAPANGA NA WAFUGAJI

Tarehe ya Kuweka: November 14th, 2023

VGS ,MTUMISHI WA HALMASHAURI WAKATWA MAPANGA NA WAFUGAJI.




Askari wa wanyamapori wa vijiji (VGS)pamoja na mtumishi wa Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo Mkoani Ruvuma wamekatwa mapanga kichwani na wafugaji.


Prisca Msuha Afisa wanyamapori na maliasili wa Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo alisema mtumishi Issa Ndomondo ambaye Cheo chake ni mhifadhi wanyamapori kutoka katika idara yake ,akiwa na dereva pamoja na askari wa wanyamapori wa vijiji wapatao 8 walitekwa na wafugaji na Kisha kuwacharangwa mapanga.


Prisca alidai mtumishi huyo akiwa na askari wasaidizi wa wanyamapori  walitekwa eneo la Nakatete kitongoji Cha milonji mamlaka ya mji mdogo wa Lusewa .


Akisimulia mkasa huo kutoka Hospitali ya Peramiho Kwa njia ya simu Issa Ndomondo Mwenyewe alidai  kuwa walitekwa na wafugaji hao wakiwa na mikuki  na kuwataka wajisalimishe .


Ndomondo alidai ofisi ilipata taarifa kutoka katika Uongozi wa jumuiya ya Kimbanda kuwa maeneo ya hifadhi yanahalibiwa na wafugaji  Kwa kukata miti  hovyo na kuendesha shughuli za kilimo na kuchunga mifugo Yao  ndani ya hifadhi.


Hata hivyo Ndomondo alisema kuwa walitoa taarifa ofisi ya Mkurugenzi

na kuanza safari ya kwenda kujiridhisha juu ya uharibifu huo lakini wakiwa wanaelekea huko ghafla ndani ya msitu walikutana na kundi la vijana  jamii ya wafugaji wenye silaha za jadi na kuwataka wasimamishe na ndipo waliposimamisha na kutakiwa wajisalimishe Kwa kushuka kwenye Hilo gari waliokuwa nalo.


Aidha Ndomondo alifafanua kuwa baada ya kushuka kwenye gari waliwahoji kuwa wanaelekea wapi na ndipo Ndomondo kudai kuwa Jumuiya ya Kimbanda imelalamika kuwa eneo lake limevamiwa na wafugaji hivyo nimetumwa kuja kuangalia uharibifu huo unaofanywa kwenye hifadhi Hali iliyoibua hasira Kwa vijana hao wa jamii za kifugaji.


Kwa Mujibu wa dereva Juma Masuwa baada ya kusimamisha gari na kujionea Hali ya vijana wa jamii ya wafugaji aliamua kutoa gari eneo Hilo na kulirudisha Nyuma walikotoka na akiwa mbali kidogo na kundi lile alishuhudia wenzake wakipigwa mapanga na Kisha wale vijana wa kifugaji kukimbia .


Masuwa  aliongeza kuwa alitakiwa na wenzake hao kurudisha gari mpaka eneo la tukio Ili waweze kupanda kuwahi hospitali na wale ambao walikuwa hawawezi walisaidiwa kupanda kwenye gari na kukimbizwa kituo Cha afya Lusewa.


Kaimu Mganga mkuu wa wilaya ya Namtumbo.Dkt. Christopher Wabwarumi alikiri  kituo Cha afya Lusewa kuwapokea wagonjwa waliocharangwa mapanga kichwani na kuwapatia huduma ya awali na Kisha  wengine kuwapa rufaa ya kwenda Hospitali kubwa Kwa matibabu na uchunguzi zaidi.


Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo Chiriku Hamis Chilumba pamoja na kuwataka watumishi kumwombea mtumishi mwenzao aweze kupona alikiri kupokea taarifa hiyo na kuiagiza idara ya wanyamapori na maliasili kuhakikisha watu wote waliopatwa na mkasa huo wanapatiwa matibabu kikamilifu .


Majeruhi waliopatwa na mkasa huo ni Issa Ndomondo mhifadhi wanyamapori,  na wengine ni askari wa wanyamapori wa vijiji Twaibu Banda,Kassimu Chai,Rashid Mbelembe,Amina Said,Mwajuma Kalumbi,Omary Komba Ramadhani Musa na Hellena Mbunda ambao Kwa Sasa wamekimbizwa hospitali ya Peramiho Kwa uchunguzi zaidi.

Mwisho.





Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA 2025 KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA NAMTUMBO January 18, 2025
  • MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI KATIKA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA NAMTUMBO MWAKA 2025 January 12, 2025
  • Ona zote

Habari Mpya

  • DC NGOLLO MALENYA AWAFARIJI WAHANGA WA RADI KATIKA KATA YA LUSEWA WILAYA YA NAMTUMBO

    February 21, 2025
  • WANANCHI NAMTUMBO WAMSHUKURU RAIS SAMIA

    January 06, 2025
  • MATREKTA aliyogawa Rais Samia yawanufaisha wananchi wa Wilaya ya Namtumbo, katika kuongeza Uzalishaji kwenye kilimo cha Kisiasa.

    January 06, 2025
  • Sukrani kwa Mhe.Rais wa wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan

    January 05, 2025
  • Ona zote

Video

HOTUBA YA WAZIRI WA TAMISEMI
Video

Kurasa za Haraka

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Halmashauri ya Songea
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Nyasa
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru

Tovuti Mashuhuri

  • TAMISEMI
  • Ikulu ya Tanzania
  • Tume ya Utumishi wa Umma
  • Baraza la Mitihani
  • Tume ya ajira Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo

    Anuani: 2 Barabara ya Boma, S.L.P 55, 57382 NAMTUMBO

    Simu ya Mezani: 0252675008

    Simu ya Mkononi: 0767519181

    Barua Pepe: ded@namtumbodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki©2021Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo. Haki zote Zimehifadhiwa.