• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Complaints |
    • Gms |
Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu ya Halmashauri
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji/Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi, Maliasili na Utalii
      • Mipango, Uchumi na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Utumishi na Utawala
      • Maji
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi na Zimamoto
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA)
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • TASAF
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Fursa za Kilimo
    • Fursa za ufugaji
    • Fursa za Madini
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Huduma za Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Mheshimiwa Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokalika
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma/Vyombo Mbalimbali vya Habari
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali

Baraza la madiwani Namtumbo lafanya uchaguzi kamati za kudumu za Halmashauri

Tarehe ya Kuweka: September 29th, 2023

BARAZA LA MADIWANI NAMTUMBO LAFANYA UCHAGUZI WA  KAMATI ZA KUDUMU ZA  HALMASHAURI.





Mwenyekiti wa Halmashauri ya  wilaya ya Namtumbo Mkoani Ruvuma Jumma Pandu alifungua kikao  Kwa kusema kuwa kikao hicho Cha baraza la madiwani kina agenda moja kuu ya kufanya uchaguzi wa kamati za kudumu za Halmashauri.


 Pandu alizitaja kamati zitakazofanya uchaguzi huo ni pamoja na kamati ya huduma ya uchumi ,ujenzi na Mazingira.,kamati ya elimu afya na  maji , kamati ya fedha uongozi na mipango ,kamati ya ukimwi pamoja na kamati ya maadili.


Kabla ya uchaguzi huo kaimu mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo Paul Ambokile alisoma barua kutoka ofisi ya Chama Cha mapinduzi ililiyokuwa ikiwasilisha jina la mgombea nafasi ya makamu mwenyekiti .


Aidha Kaimu Mkurugenzi alisoma Jina la Lukas Njogopa kuwa ni jina lililoteuliwa na Chama  Cha Mapinduzi kugombea nafasi ya makamu mwenyekiti na kuwashauri wajumbe kupiga kura ya ndio au hapana Kwa kuwa mgombea nafasi hiyo ni mtu mmoja na kutoka kwenye Chama kimoja.


Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo aliwataka waheshimiwa madiwani kupiga kura ambapo kati ya madiwani 28 kura za ndiyo zilikuwa 28 na hapakuwa na kura yoyote ya hapana na kumfanya Lukas Njogopa kutangazwa kuwa ni makamu mwenyekiti wa Halmashauri ya Namtumbo Kwa kipindi Cha mwaka mmoja .


Baada  ya zoezi hilo mwenyekiti alizitaka Kila kamati kufanya uchaguzi wa nafasi ya mwenyekiti wa kamati Ili kumpata mwenyekiti wa kamati aliyechaguliwa na wajumbe wa kamati husika.


Kaimu mkurugenzi Paul Ambokile alisoma matokeo ya uchaguzi  kwa nafasi ya mwenyekiti kutoka Kila kamati ambapo alimtangaza Charles Chengula aliyepata kura 7 kuwa mwenyekiti wa kamati ya huduma ya uchumi ujenzi na mazingira Kwa kumshinda mpinzani wake Dani Nyambo aliyepata kura 6 kati ya kura 13 zilizopigwa.


Alimtangaza Said Zidadu kuwa mwenyekiti wa kamati ya Elimu afya na maji aliyepata kura 9 baada ya kuwashinda wapinzani wake Isdori Nyati aliyepata kuwa 3 na Kassimu Gunda aliyepata kura 1


Hata hivyo Ambokile alimtangaza Paul Fussi kuwa mwenyekiti wa kamati ya maadili Kwa kumshinda mpinzani wake Mrisho Mbawala aliyepata kura 1 kati ya kura 6 zilizopigwa na kumalizia na kamati ya ukimwi ambapo kamati hii Kwa Mujibu wa miongozo anayekuwa makamu mwenyekiti ndiye anakuwa mwenyekiti wa kamati hiyo ambaye ni Lukas Njogopa.


Zuberi Lihuwi mwenyekiti wa Chama Cha mapinduzi wilaya ya Namtumbo aliwaambia waheshimiwa madiwani kwenda kutekeleza majukumu Yao Kwa Ari na ustawi wa Halmashauri na Kwa kuzingatia mawazo ya watu waliowatuma.


Lihuwi Pia aliwataka madiwani hao kuisimamia Halmashauri ambayo alidai inachangamoto nyingi na hazina ulazima wa kuendelea kuwepo alisema Lihuwi.


Lakini pia Lihuwi aliwataka madiwani hao kwenda kufanya kazi katika maeneo Yao Kwa kuwa Chama kinategemea uwajibikaji wao katika nafasi zao na kuwaagiza madiwani hao kusimamia maamuzi Yao.


Amina Tindwa Afisa Serikali za mitaa kutoka katika ofisi ya Katibu tawala Mkoa wa Ruvuma aliwataka madiwani kwenda kuwa tumikia wananchi Kwa kusikiliza kero na kuzipatia majawabu Kwa kufanya mikutano ya hadhara katika maeneo Yao.


kikao Cha baraza la madiwani kilifanyika Leo katika ukumbi wa Halmashauri ambapo kabla ya kumaliza kikao hicho mwenyekiti aliwatangaza wajumbe aliowateua watakaoungana na wenyeviti wa kamati kuwa wajumbe wa kamati ya fedha uongoxi na mipango kuwa ni Zamania Komba,Remna Nchimbi,Salimu Nyoni na Isdori Nyati  kuungana na wenyeviti wa kamati kuwa wajumbe wa kamati ya fedha uongozi na mipango.

Mwisho.





Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA 2025 KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA NAMTUMBO January 18, 2025
  • MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI KATIKA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA NAMTUMBO MWAKA 2025 January 12, 2025
  • Ona zote

Habari Mpya

  • DC NGOLLO MALENYA AWAFARIJI WAHANGA WA RADI KATIKA KATA YA LUSEWA WILAYA YA NAMTUMBO

    February 21, 2025
  • WANANCHI NAMTUMBO WAMSHUKURU RAIS SAMIA

    January 06, 2025
  • MATREKTA aliyogawa Rais Samia yawanufaisha wananchi wa Wilaya ya Namtumbo, katika kuongeza Uzalishaji kwenye kilimo cha Kisiasa.

    January 06, 2025
  • Sukrani kwa Mhe.Rais wa wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan

    January 05, 2025
  • Ona zote

Video

HOTUBA YA WAZIRI WA TAMISEMI
Video

Kurasa za Haraka

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Halmashauri ya Songea
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Nyasa
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru

Tovuti Mashuhuri

  • TAMISEMI
  • Ikulu ya Tanzania
  • Tume ya Utumishi wa Umma
  • Baraza la Mitihani
  • Tume ya ajira Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo

    Anuani: 2 Barabara ya Boma, S.L.P 55, 57382 NAMTUMBO

    Simu ya Mezani: 0252675008

    Simu ya Mkononi: 0767519181

    Barua Pepe: ded@namtumbodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki©2021Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo. Haki zote Zimehifadhiwa.