• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Complaints |
    • Gms |
Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu ya Halmashauri
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji/Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi, Maliasili na Utalii
      • Mipango, Uchumi na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Utumishi na Utawala
      • Maji
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi na Zimamoto
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA)
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • TASAF
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Fursa za Kilimo
    • Fursa za ufugaji
    • Fursa za Madini
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Huduma za Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Mheshimiwa Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokalika
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma/Vyombo Mbalimbali vya Habari
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali

BARAZA LA WAFANYAKAZI NAMTUMBO LAPITISHA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI 2022/2023

Tarehe ya Kuweka: January 13th, 2022


Baraza la wafanyakazi katika Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma limepitisha mapendekezo ya mpango na bajeti wa Halmashauri  ya wilaya ya Namtumbo kwa mwaka wa fedha unaoanzia julai mosi 2022 na kuishia  juni 30,2023.

Akiwasilisha bajeti hiyo kwenye kikao cha baraza la wafanyakazi , kaimu afisa mipango wa Halmashauri  ya wilaya ya Namtumbo Mohamed Ninje alisema halmashauri hiyo inakisia kukusanya na kupokea jumla ya shilingi 29,824,217,000 kutoka vyanzo vya ndani,ruzuku kutoka serikali kuu na wadau  wa maendeleo.

Ninje alidai  Halmashauri  inakisia kukusanya shilingi 1,984,000,000 kutoka vyanzo vya mapato ya ndani, ruzuku kutoka serikali kuu shilingi  23,015,526,000 na shilingi 4,131,528,000 kutoka kwa wadau wa maendeleo.

Aidha  Ninje pia  alifafanua mapendekezo ya matumizi ya bajeti hiyo kuwa shilingi  18,043,444,000 itatumika kwa ajili ya mishahara, huku shilingi 2,663,849,000 kwa ajili ya matumizi mengineyo na shilingi 9,116,924,000 kwa ajili ya miradi ya maendeleo.

Afisa elimu ,elimu maalumu  wa Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo  Thabiti  Mponda aliomba kuongezwa kwa bajeti katika kitengo cha elimu maalumu kwa kuwa mahitaji ya watu wenye mahitaji maalumu yanazidi kuongezeka lakini  bajeti  imeendelea kumebaki palepale.

Mponda alisikitika kusikia katika bajeti hiyo Halmashauri itajikita katika kuboresha utoaji  wa huduma kwa shule mbili maalumu za msingi badala  ya shule  nne za msingi maalumu zilizopo katika Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo na kuomba kuongezwa bajeti na kuweka shule nne maalumu badala ya shule mbili .

Mwalimu Rashidi Shaban Mussa (Malimba) alishangazwa na taarifa ya ukusanyaji wa ushuru kituo kikuu cha mabasi cha wilaya ya Namtumbo na kudai kuwa licha ya wadau kushauri katika vikao vikiwemo vya baraza la biashara wilaya ambaye yeye ni mjumbe hakuna jitihada za maksudi za uongozi kuyafanyia kazi mapendekezo ya wadau katika kuongeza ukusanyaji wa mapato katika stendi ya mabasi wilaya ya Namtumbo.

Afisa mipango wa Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo Amos Kanige alisema swala la usimamizi na ufunguzi wa stendi ya wilaya limekamilika hivyo muda wowote kuanzia sasa stendi hiyo itafunguliwa na kuongeza mapato ya Halmashauri  ya wilaya ya Namtumbo ambapo magari yatabaki katika stendi rasmi na kupakia abiria hapo tofauti na hivi sasa wasafirishaji abiria hutumia stendi zisizorasmi na kukwepa ulipaji wa ushuru .

Kikao cha baraza la wafanyakazi kupitia mapendekezo ya mpango na bajeti ya Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo kilitanguliwa na uchaguzi wa katibu wa baraza la wafanyakazi na  katika uchaguzi huo wagombea walikuwa wawili  , Shaibu Majiwa Afisa elimu watu wazima na Edigna Muhule afisa mifugo ambapo  Shaibu Majiwa aliibuka mshindi kwa kura 27 dhidi ya kura 21 alizopata mshindani wake Edigna Mhule huku wapiga kura walikuwa 50 ikiwa katika upigaji  kura hizo 2 ziliharibika.

Kaimu mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo Paul  Ambokile pamoja na mambo mengine aliwashukuru wajumbe wa Baraza la wafanyakazi wilayani Namtumbo  kwa kupitia kipengele kwa kipengele na kuridhia kupitisha mapendekezo ya bajeti 2022/2023 na kuhaidi ofisi yake itaongeza ushirikishwaji kwa jamii  katika mpango na bajeti ya Halmashauri hiyo ili kuongeza uwazi,ushirikishwaji ,uwajibikaji  katika kuleta maboresho katika  huduma za jamii.

Mwisho.

Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA YA WAOMBAJI WA KAZI YA MUDA YA SENSA WALIOFAULU USAILI NA KUITWA KWENYE MAFUNZO July 27, 2022
  • TAARIFA KWA UMMA June 27, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WAOMBAJI WA KAZI YA MUDA YA SENSA WALIOFAULU USAILI NA KUITWA KWENYE MAFUNZO July 27, 2022
  • MABADILIKO YA TAREHE YA KUFANYA USAILI June 22, 2022
  • Ona zote

Habari Mpya

  • ORODHA YA MAJINA YA WASIMAMIZI WA MAUDHUI, WASIMAMIZI WA TEHAMA NA MAKARANI WA SENSA WALIOFAULU USAILI WA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA YA SENSA NA KUITWA KWENYE MAFUNZO

    July 27, 2022
  • HALMASHAURI NAMTUMBO YAGAWA PIKIPIKI 38 KWA MAAFISA UGANI NA USHIRIKA

    June 24, 2022
  • MABADILIKO YA TA TAREHE YA KUFANYA USAILI

    June 22, 2022
  • DC NAMTUMBO ATANGAZA KIAMA WATAKAOPOTOSHA ZOEZI LA SENSA

    June 02, 2022
  • Ona zote

Video

HOTUBA YA WAZIRI WA TAMISEMI
Video

Kurasa za Haraka

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Halmashauri ya Songea
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Nyasa
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru

Tovuti Mashuhuri

  • TAMISEMI
  • Ikulu ya Tanzania
  • Tume ya Utumishi wa Umma
  • Baraza la Mitihani
  • Tume ya ajira Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo

    Anuani: S.L.P 55 NAMTUMBO

    Simu ya Mezani: 0252675008

    Simu ya Mkononi: 0765142640

    Barua Pepe: ded@namtumbodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki©2021Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo. Haki zote Zimehifadhiwa.