• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Complaints |
    • Gms |
Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu ya Halmashauri
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji/Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi, Maliasili na Utalii
      • Mipango, Uchumi na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Utumishi na Utawala
      • Maji
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi na Zimamoto
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA)
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • TASAF
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Fursa za Kilimo
    • Fursa za ufugaji
    • Fursa za Madini
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Huduma za Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Mheshimiwa Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokalika
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma/Vyombo Mbalimbali vya Habari
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali

DC NAMTUMBO AKABIDHI WALIMU JUMLA YA VISHIKWAMBI 717

Tarehe ya Kuweka: January 10th, 2023

DC NAMTUMBO AWAKABIDHI WALIMU VISHIKWAMBI 717.

Mkuu wa wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma Dkt Julius Kenneth Ningu amewakabidhi walimu wa shule za msingi na sekondari  jumla ya vishikwambi 717.

Akizungumza na walimu hao kabla ya kukabidhi vishikwambi hivyo Dkt Ningu alisema serikali ina nia njema ya kutaka kuwaboreshea walimu mazingira ya ufundishaji,ujifunzaji,ufuatiliaji na usimamizi wa elimu kwa kutumia vishikwambi hivyo.

Dkt Ningu alidai kuwepo kwa waratibu elimu kata waliopewa pikipiki na serikali kwa ajili ya kufuatilia maswala ya elimu lakini wakizitumia pikipiki hizo kwa kufanyia kazi zao binafsi za shambani tofauti na malengo ya serikali na kuwataka walimu waliopewa vishikwambi hivyo kutumia kadiri ya malengo ya serikali.

Zoezi la ugawaji wa vishikwambi hivyo liliambatana na utoaji wa taarifa ya matokeo ya kuhitimu darasa la saba ,matokeo ya upimaji  darasa la  nne  na kidato cha pili kwa mwaka 2022.

Afisa elimu shule za msingi wa Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo Juma Fulluge katika taarifa yake alidai matokeo ya darasa la saba kwa mwaka 2022 yameshuka kwa asilimia 11ukilinganisha na mwaka 2021 huku waliofanya mitihani ya kuhitimu darasa la saba kwa mwaka 2022 walikuwa 7409 kati ya 7677 waliosajiliwa kufanya mitihani hiyo sawa na asilimia 96.5

Fulluge kwa upande wake pia alitoa taarifa ya upimaji wa matokeo ya darasa la nne na kudai kuwa kwa mwaka huu 2022 ufaulu wa wanafunzi umekuwa wa asilimia 75 .24 na mwaka 2021 asilimia 86.7 huku mwaka 2020 asilimia 97.89.

Hata hivyo afisa elimu sekondari wa Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo Michael Lyambilo katika taarifa yake alisema ufaulu wa wanafunzi wa kidato cha pili kwa mwaka 2022 umekuwa wa asilimia70.45 ambapo mwaka 2021 ulikuwa asilimia 80.10 na mwaka 2020 ulikuwa asilimia 89.18.

Mkuu wa shule ya sekondari Korido, Oskar Komba alitumia nafasi hiyo kutoa changamoto inayosababisha wanafunzi kufeli ni umbali uliopo kati ya shule na vijiji wanakotoka wanafunzi wanaosoma sekondari kuwa, ni changamoto kubwa kwani wanafunzi hutumia kitambo kirefu kutembea kufika shuleni na wakifika shuleni huwa wamechoka.

Komba aliiomba serikali kuhakikisha jamii inahamasishwa kujenga mabweni ya wasichana na wavulana ili wanafunzi hao wabaki shuleni na kutumia muda wao mwingi katika kujikita na masomo.

Mwalimu Elias Ngonyani wa shule ya msingi Mandela alilalamikia kitendo cha kata,wilaya,na mkoa kutegemea fedha kutoka shuleni ili kuweza kuandaa mitihani mbalimbali ili hali fedha zinazopatikana katika shule hizo hazikidhi mahitaji ya shule na kuomba kata ,wilaya na mkoa iandae mitihani bila kutegemea michango ya fedha kutoka shuleni.

Shule  binafsi za sekondari katika matokeo ya kidato cha pili zimeongoza kushika nafasi ya kwanza mpaka nafasi ya tano ,nafasi ya kwanza mpaka ya tatu kwa matokeo ya darasa la nne na nafasi ya kwanza mpaka ya pili kwa darasa la saba 2022.

MWISHO.

Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA YA WAOMBAJI WA KAZI YA MUDA YA SENSA WALIOFAULU USAILI NA KUITWA KWENYE MAFUNZO July 27, 2022
  • TAARIFA KWA UMMA June 27, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WAOMBAJI WA KAZI YA MUDA YA SENSA WALIOFAULU USAILI NA KUITWA KWENYE MAFUNZO July 27, 2022
  • MABADILIKO YA TAREHE YA KUFANYA USAILI June 22, 2022
  • Ona zote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NAMTUMBO LAPITISHA MAPENDEKEZO YA MPANGO WA BAJETI 2023/2024

    January 30, 2023
  • MAADHIMISHO YA KUZALIWA KWA RAIS SAMIA YAAMBATANA NA UPANDAJI WA MITI RUVUMA

    January 27, 2023
  • SHULE 16 NAMTUMBO ZANUFAIKA NA WALIMU WA MAZOEZI YA KUFUNDISHA

    January 26, 2023
  • MIFUGO MINGINE 508 YAKAMATWA NAMTUMBO

    January 25, 2023
  • Ona zote

Video

HOTUBA YA WAZIRI WA TAMISEMI
Video

Kurasa za Haraka

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Halmashauri ya Songea
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Nyasa
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru

Tovuti Mashuhuri

  • TAMISEMI
  • Ikulu ya Tanzania
  • Tume ya Utumishi wa Umma
  • Baraza la Mitihani
  • Tume ya ajira Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo

    Anuani: S.L.P 55 NAMTUMBO

    Simu ya Mezani: 0252675008

    Simu ya Mkononi: 0765142640

    Barua Pepe: ded@namtumbodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki©2021Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo. Haki zote Zimehifadhiwa.