• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Complaints |
    • Gms |
Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu ya Halmashauri
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji/Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi, Maliasili na Utalii
      • Mipango, Uchumi na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Utumishi na Utawala
      • Maji
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi na Zimamoto
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA)
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • TASAF
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Fursa za Kilimo
    • Fursa za ufugaji
    • Fursa za Madini
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Huduma za Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Mheshimiwa Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokalika
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma/Vyombo Mbalimbali vya Habari
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali

Wadau Namtumbo Watoa Maagizo mazito mfumo wa stakabadhi ghalani

Tarehe ya Kuweka: April 19th, 2024

WADAU NAMTUMBO WATOA MAAZIMIO MAZITO KUSIMAMIA MFUMO WA STAKABADHI GHALANI.

Kikao Cha wadau katika Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo Mkoani Ruvuma  kilichoketi tarehe 18.4.2024  katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo kilitoa Maazimio mazito katika kusimamia mfumo wa stakabadhi ghalani Wilayani humo.

Awali akisoma taarifa ya uendeshaji mfumo wa stakabadhi ghalani  Kwa msimu uliopita wa mwaka 2022/2023 Afisa kilimo,mifugo na uvuvi wa Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo Paul Ambokile aliwaambia wadau hao kuwa mauzo kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani umewanufaisha wakulima Kwa kiasi kikubwa. Kwa kuuza mazao Yao Kwa bei nzuri na kuwa na uhakika na soko Kwa mazao Yao.


Hata hivyo Ambokile alisema mfumo wa stakabadhi ya ghala ni mfumo unaotumika kisheria chini ya sheria namba 10 ya mwaka 2005 na kutekelezwa Kwa kanuni za mfumo za mwaka 2006.


Issa Issa Ntine mkulima kutoka chama Cha msingi Mliwasi Wilayani humo alisema mfumo wa stakabadhi ghalani ni mzuri Kwa mkulima wa kipato Cha chini lakini akaziomba Taasisi za kibenki kuwasaidia wakulima Kwa kutofunga akaunti zao Kwa kuwa fedha zao ni za msimu ili kuwaondolea usumbufu mara wauzapo mazao Yao kuambiwa akaunti zao zimelala au kufungwa Kwa kutoweka fedha muda mrefu na kuleta usumbufu mkubwa Kwa wakulima hao na wakati mwingine wakulima wanalalamikia kuchelewa kulipwa fedha zao kumbe ni kutokana na Changamoto hizo.


Asedi Kaporo mwenyekiti wa chama Cha msingi Namtumbo pamoja na kusema kuwa mfumo ni mzuri alikiomba chama kikuu SONAMCU kutumia zoni katika kusambaza vifungashio badala ya vyama vya msingi vyote kufuata vifungashio katika eneo Moja ili kurahisisha usafirishaji na upatikani wake Kwa uharaka.


Kaporo alipendekeza zoni za kusambaza vifungashio ziwe nne ambapo alipendekeza zoni ya Lusewa, Namtumbo ,Mgombasi na Hanga ili kurahisisha usambazaji na upatikanaji wa vifungashio Kwa wakulima.


Diwani wa kata ya Mkongo  Daniel Nyambo Pamoja na kusema mfumo wa stakabadhi ghalani unawanufaisha wakulima aliwaambia wadau hao kuwa mfumo umeingiliwa na wafanyabiashara ambao hukopesha wakulima fedha ndogo na hulipwa ufuta mwingi na wao kuuza katika mfumo wa stakabadhi ya ghala na kujipatia pesa nyingi.


Nyambo alisikitishwa na kitendo Cha wafanyabiashara katika kata yake ya Mkongo kuwakopesha wakulima fedha shilingi 50,000 na kulipwa ufuta kilo 100 ambapo waliuza katika mfumo wa stakabadhi ghalani na kujipatia 400,000 Kwa bei ya mwanzo Kwa msimu wa 2022/2023.


Nyambo alidai juhudi za maksudi zinahitajika hasa Kwa Taasisi zetu za kibenki kuwakopesha wakulima fedha na pembejeo ili waweze kulima Kwa Tija badala ya kuwa watumwa wa watu wengine.


Diwani wa kata ya Kitanda Charles Chengula alisisitiza suala la ukusanyaji wa mapato, Madiwani ,viongozi wa Serikali kuwa na msimamo wa Pamoja kudhibiti  utoroshaji wa mazao na ushuru wa Halmashauri  


Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo Ngollo Malenya aliwaambia wadau kuwa mfumo wa stakabadhi ghalani umewawezesha wakulima  wa Wilaya ya Namtumbo kupata bei nzuri Kwa mazao ya ufuta,mbaazi na soya Pamoja na kuwa na uhakika wa soko.


Aliwaagiza viongozi wa vyama vya msingi kuhakikisha wanasimamia mfumo Kwa uadilifu mkubwa na kinyume Cha hapo serikali itasimamia haki Kwa wananchi na kuwataka viongozi hao kuondoa dhana kuwa mambo ya ushirika hayaingiliwi .


Hata hivyo Malenya alimwagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Namtumbo kuhakikisha anawaandikia barua watendaji wa kata na vijiji kudhibiti ununuzi holela wa mazao ya wakulima Bila kufuata utaratibu kanuni na sheria zilizopo.


Malenya aliongeza kuwa jitihada za Pamoja za kusimamia ukusanyaji wa mapato na kusimamia kudhibiti utoroshaji wa mapato katika Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo unahitajika Sana.


Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo Philemon Mwita Magesa aliwataka wadau kushirikiana katika kuhakikisha mfumo wa stakabadhi ghalani una wanufaisha wananchi wa Namtumbo.


Magesa alidai kuwepo Kwa wafanyabiashara wanaonunua ufuta Kwa wakulima na wafanyabiashara wanaokopesha fedha Kwa wakulima Kwa fedha ndogo na wakati wa masoko Kwa mfumo wa stakabadhi ghalani unapoanza wafanyabiashara hao hupeleka ufuta na kulipwa fedha nyingi  ambazo nazo hazibaki Namtumbo huondoka  na kwenda kufanya matumizi maeneo mengine nje ya Namtumbo.


Magesa aliwaambia wadau waliohudhuria kikao hicho kuwa kitendo hicho kina madhara makubwa Kwa maendeleo ya Namtumbo hivyo akawataka wadau kushirikiana Kwa Pamoja kusimamia mfumo wa stakabadhi ghalani Kwa kuwataka wakulima wenyewe wa Namtumbo kuuza mazao Yao Kwa mfumo wa stakabadhi ghalani ili fedha watakazopata zitabaki Namtumbo Kwa maendeleo ya Namtumbo alisema Magesa.


Viongozi wa vyama vya msingi 47 katika Wilaya ya Namtumbo , viongozi wa vikundi vya wakulima ,wanunuzi wa mazao ,viongozi wa wafanyabiashara ,kamati ya Ulinzi na usalama ya Wilaya ya Namtumbo ,wakuu wa idara , Taasisi za kibenki  Pamoja na wamiliki wa maghala walihudhuria kikao hicho ..

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA 2025 KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA NAMTUMBO January 18, 2025
  • MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI KATIKA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA NAMTUMBO MWAKA 2025 January 12, 2025
  • Ona zote

Habari Mpya

  • DC NGOLLO MALENYA AWAFARIJI WAHANGA WA RADI KATIKA KATA YA LUSEWA WILAYA YA NAMTUMBO

    February 21, 2025
  • WANANCHI NAMTUMBO WAMSHUKURU RAIS SAMIA

    January 06, 2025
  • MATREKTA aliyogawa Rais Samia yawanufaisha wananchi wa Wilaya ya Namtumbo, katika kuongeza Uzalishaji kwenye kilimo cha Kisiasa.

    January 06, 2025
  • Sukrani kwa Mhe.Rais wa wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan

    January 05, 2025
  • Ona zote

Video

HOTUBA YA WAZIRI WA TAMISEMI
Video

Kurasa za Haraka

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Halmashauri ya Songea
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Nyasa
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru

Tovuti Mashuhuri

  • TAMISEMI
  • Ikulu ya Tanzania
  • Tume ya Utumishi wa Umma
  • Baraza la Mitihani
  • Tume ya ajira Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo

    Anuani: 2 Barabara ya Boma, S.L.P 55, 57382 NAMTUMBO

    Simu ya Mezani: 0252675008

    Simu ya Mkononi: 0767519181

    Barua Pepe: ded@namtumbodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki©2021Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo. Haki zote Zimehifadhiwa.