• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Complaints |
    • Gms |
Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu ya Halmashauri
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji/Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi, Maliasili na Utalii
      • Mipango, Uchumi na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Utumishi na Utawala
      • Maji
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi na Zimamoto
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA)
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • TASAF
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Fursa za Kilimo
    • Fursa za ufugaji
    • Fursa za Madini
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Huduma za Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Mheshimiwa Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokalika
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma/Vyombo Mbalimbali vya Habari
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali

Wakulima Namtumbo WAPATIWA MAFUNZO ya sumukuvu

Tarehe ya Kuweka: December 9th, 2023


WAKULIMA NAMTUMBO WAPATIWA MAFUNZO YA SUMUKUVU



Wakulima wa vijiji kumi  katika Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo Mkoani Ruvuma wamepatiwa mafunzo ya Kudhibiti sumukuvu  kuanzia hatua ya uandaaji shamba, ulimaji,utiaji mbolea na hatua za kufuata katika uvunaji.


Akiongea na wakulima wa wilaya  ya Namtumbo Dafrosa Jerome Afisa kilimo kutoka wizara ya kilimo aliwaambia wakulima hao kuwa moja ya njia ya kudhibiti Sumukuvu ni kufuata hatua za kilimo bora pamoja na kutumia dawa ya kuua wadudu wanaosababisha sumukuvu.(aflasafe)


Dafrosa pamoja na mambo mengine aliwafundisha wakulima hao Kwa vitendo namna ya kulima,kupanda ,utiaji wa mbolea , utiaji dawa ya kuua wadudu wanaosababisha Sumukuvu pamoja na hatua za uvunaji Ili kuwakwepa wadudu wanaosababisha Sumukuvu kutoingia katika mazao ya mkulima.


Michael Gambi afisa kilimo wa Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo ambaye pia ni mratibu wa kudhibiti sumu kuvu katika Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo alitaja vijiji ambavyo vikundi vyake vimepatiwa mafunzo hayo ni Utwango,Msindo,Nahoro,Mawa,na Luhimbalilo.


Gambi Alivitaja vijiji vingine ambavyo vimepatiwa  mafunzo hayo kuwa ni Naikesi,Nangero,Mfuate -likuyu, Namtumbo pamoja na Minazini vyote vya wilaya hiyo ya Namtumbo.


Pamoja  na hayo Gambi alidai mafunzo hayo yaliambatana na ugawaji wa mbegu za mahindi aina ya ASA  T105 Kwa wakulima 30 Kwa Kila Kijiji ,mbolea ya kupandia  aina ya DAP Kwa mashamba darasa ,kamba ,pamoja na kiatilifu (Atlasafe) kuuua wadudu wanaosababisha Sumukuvu kwenye mazao.


Naimu Saweji Luambano mkazi wa Kijiji Cha Nangero wilayani Namtumbo alidai mafunzo hayo yamewasaidia w inakulima kujua kanuni Bora za kilimo lakini pia kujua namna ya kudhibiti mazao yasiathirike na sumukuvu kuanzia hatua ya kuandaa shamba mpaka kuvuna .


Luambano alifafanua kuwa wakulima wamefundishwa kutenganisha mahindi mabovu na mazuri Ili kuepuka sumukuvu katika mazao Ili kuepukana na homa zitokanazo na kula vyakula zilizokuwa na sumukuvu.


Pamoja na kuishukuru Serikali kuwaletea wakulima hao mafunzo. Luambano aliiomba Serikali kuendelea Kutoa elimu hiyo Kwa wakulima wengi na katika vijiji vyote vya wilaya ya Namtumbo tofauti na ilivyo hivi Sasa ambapo ni vijiji vichache ndivyo vimepatiwa mafunzo hayo.


Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo Ina jumla ya vijiji 66 na mamlaka ya miji midogo miwili  na kati ya vijiji hivyo vijiji 10 vimepatiwa mafunzo ya Sumu kuvu.

Mwisho.



















Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA 2025 KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA NAMTUMBO January 18, 2025
  • MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI KATIKA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA NAMTUMBO MWAKA 2025 January 12, 2025
  • Ona zote

Habari Mpya

  • DC NGOLLO MALENYA AWAFARIJI WAHANGA WA RADI KATIKA KATA YA LUSEWA WILAYA YA NAMTUMBO

    February 21, 2025
  • WANANCHI NAMTUMBO WAMSHUKURU RAIS SAMIA

    January 06, 2025
  • MATREKTA aliyogawa Rais Samia yawanufaisha wananchi wa Wilaya ya Namtumbo, katika kuongeza Uzalishaji kwenye kilimo cha Kisiasa.

    January 06, 2025
  • Sukrani kwa Mhe.Rais wa wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan

    January 05, 2025
  • Ona zote

Video

HOTUBA YA WAZIRI WA TAMISEMI
Video

Kurasa za Haraka

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Halmashauri ya Songea
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Nyasa
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru

Tovuti Mashuhuri

  • TAMISEMI
  • Ikulu ya Tanzania
  • Tume ya Utumishi wa Umma
  • Baraza la Mitihani
  • Tume ya ajira Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo

    Anuani: 2 Barabara ya Boma, S.L.P 55, 57382 NAMTUMBO

    Simu ya Mezani: 0252675008

    Simu ya Mkononi: 0767519181

    Barua Pepe: ded@namtumbodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki©2021Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo. Haki zote Zimehifadhiwa.