• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Complaints |
    • Gms |
Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu ya Halmashauri
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji/Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi, Maliasili na Utalii
      • Mipango, Uchumi na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Utumishi na Utawala
      • Maji
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi na Zimamoto
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA)
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • TASAF
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Fursa za Kilimo
    • Fursa za ufugaji
    • Fursa za Madini
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Huduma za Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Mheshimiwa Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokalika
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma/Vyombo Mbalimbali vya Habari
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali

ZIARA YA DC NAMTUMBO YATAWALIWA NA MALALAMIKO YA WAFUGAJI

Tarehe ya Kuweka: May 3rd, 2023

ZIARA YA DC NAMTUMBO YATAWALIWA  NA MALALAMIKO YA WAFUGAJI.

Mkuu wa wilaya ya Namtumbo Mkoani  Ruvuma  Ngollo  Ng’waniduhu Malenya anafanya ziara ya kuzungumza na wananchi wa wilaya ya Namtumbo  kwa kusikiliza kero  zao na kuzipatia majawabu kero hizo.

Ziara hiyo imeanza leo tarehe 3mei 2023 kwa kuzungumza na wananchi wa kijiji cha Lingusenguse ,Sasawala,Amani  pamoja na kijiji cha Ligunga ambapo kero kubwa kwa wananchi wa vijiji hivyo ilikuwa kero ya wafugaji katika mazingira ambayo wananchi wa vijiji hivyo wanafanya shughuli za kilimo.

Mwenyekiti wa kijiji cha Sasawala Saidi Mbele alimwomba mkuu wa wilaya kibali cha kuwaondoa wafugaji kwa nguvu ili kuwafanya wananchi wa kijiji chake kufanya shughuli za kilimo bila kuhofia wafugaji kulisha mazao yao .

Mbele alidai wakulima wa kijiji chake wameomba msaada ngazi ya wilaya na mkoa kwa kuomba msaada wa kuwaondoa wafugaji bila mafanikio na kumwomba mkuu wa wilaya huyo kibali cha kutumia wananchi  wake kuwaondoa wafugaji hao kwa nguvu.

Omari Yahaya wa kijiji cha Amani wilayani humo alimwambia mkuu wa wilaya huyo kuwa wananchi wanaolima katika maeneo ya hifadhi huondolewa kwa nguvu lakini wafugaji wengi wapo katika hifadhi hizo na hawaondolewi kwa nguvu.

Hata hivyo Yahaya alidai maeneo yaliyotengwa na vijiji kwa ajili ya mapito ya wanyama (ushoroba) kwa sasa maeneo hayo kwa sasa wanyama wametoweka kuwakimbia wafugaji walioenea katika maeneo hayo .

Afisa mifugo wa Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo Paul  Ambokile aliwaambia wananchi hao utaratibu wa kuufuata katika kuwapokea wageni katika maeneo ya vijiji vyao lakini akawahatarisha viongozi wa vijiji kuheshimu msimamo na maamuzi ya wilaya kuwa hakuna maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya wafugaji katika wilaya ya Namtumbo.

Afisa maliasili na usafi wa mazingira Priska Msuha alikiri kuwepo kwa wafugaji wengi katika maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya mapito ya wanyama (ushoroba) na maeneo ya misitu na kufanya wanyama wakimbie maeneo hayo .

Mkuu wa wilaya ya Namtumbo pamoja na mambo mengine aliwahimiza viongozi wa vijiji kuwa wenye mamlaka ya kulinda ardhi ya kijiji ni kijiji chenyewe na kutofanya hivyo kutafanya wafugaji waendelee kuharibu mazingira ya vijiji na kutengeneza migogoro

Ngollo aliwaambia wananchi hao kuwa wafugaji  hawajawahi kuwa watunzaji wa mazingira bali wao wamekuwa waharibifu wakubwa wa mazingira  na kuwataka viongozi wa vijiji kujua  kuwa maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya wafugaji ni wilaya ya Tunduru na sio katika wilaya ya Namtumbo.

Hata hivyo mkuu wa wilaya huyo alisema utaratibu wa kuwaondoa wafugaji hao katika maeneo yasiyorasmi unaendelea na kuwataka viongozi wa vijiji kushirikiana na ofisi yake katika kufanikisha jambo hilo.

Ziara ya mkuu wa wilaya huyo kutembelea vijiji vya wilaya ya Namtumbo imeanza leo tarehe 3mei  na itamalizika tarehe 8 mei mwaka huu 2023 kwa kuzungumza na wananchi wa vijiji 66 na mamlaka ya miji midogo miwili ya Lusewa na Namtumbo.

Mwisho.

Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA KWA WATENDAJI WA VIJIJI NA MADEREVA April 13, 2023
  • TANGAZO LA AJIRA KWA WATENDAJI WA VIJIJI NA MADEREVA April 13, 2023
  • ORODHA YA MAJINA YA WAOMBAJI WA KAZI YA MUDA YA SENSA WALIOFAULU USAILI NA KUITWA KWENYE MAFUNZO July 27, 2022
  • TANGAZO LA AJIRA KWA WATENDAJI WA VIJIJI NA MADEREVA April 13, 2023
  • Ona zote

Habari Mpya

  • MNADA WA UFUTA WAIBUA SHANGWE NA NDEREMO KWA WAKULIMA NAMTUMBO

    May 25, 2023
  • DC NAMTUMBO AWAAMURU WAFUGAJI KUONDOKA KWA MASLAHI MAPANA YA TAIFA

    May 08, 2023
  • DC NAMTUMBO AWAONYA WAFUGAJI

    May 05, 2023
  • DC NAMTUMBO AWASIMAMISHA KAZI WENYEVITI WATANO WA VITONGOJI

    May 04, 2023
  • Ona zote

Video

HOTUBA YA WAZIRI WA TAMISEMI
Video

Kurasa za Haraka

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Halmashauri ya Songea
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Nyasa
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru

Tovuti Mashuhuri

  • TAMISEMI
  • Ikulu ya Tanzania
  • Tume ya Utumishi wa Umma
  • Baraza la Mitihani
  • Tume ya ajira Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo

    Anuani: S.L.P 55 NAMTUMBO

    Simu ya Mezani: 0252675008

    Simu ya Mkononi: 0765142640

    Barua Pepe: ded@namtumbodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki©2021Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo. Haki zote Zimehifadhiwa.