• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Complaints |
    • Gms |
Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu ya Halmashauri
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji/Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi, Maliasili na Utalii
      • Mipango, Uchumi na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Utumishi na Utawala
      • Maji
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi na Zimamoto
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA)
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • TASAF
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Fursa za Kilimo
    • Fursa za ufugaji
    • Fursa za Madini
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Huduma za Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Mheshimiwa Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokalika
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma/Vyombo Mbalimbali vya Habari
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali

mikakati iongezwe ya kuwataka wananchi wapime vvu kwa hiari

Tarehe ya Kuweka: December 2nd, 2020

MIKAKATI  IONGEZWE  YA  KUWATAKA  WANANCHI WAPIME  VVU  KWA HIARI.


Katibu  tawala  wa wilaya  ya  Namtumbo  Aden  Nchimbi  alimwakilisha mKuu wa Mkoa  wa Ruvuma  Christina  Mndeme katika  maadhimisho  ya Siku  ya ukimwi  duniani  ambapo  kimkoa yalifanyika uwanja  wa  taifa wilaya ya  Namtumbo .

Katika hotuba yake  kwa wananchi  amewataka  kuongeza jitihada  za kuwa  na mazoea  ya kupima virusi vya ukimwi  mara kwa mara  ili  kuishi  maisha  yenye faraja  pale  unapogundulika kuatdhirika  na virusi hivyo  kwa  kuanza  kupata  dawa  mapema na kuijiongezea  muda wa  kuishi  na wale ambao watabainika kuwa salama  wachukue  tahadhari  na kubadili mienendo ya maisha  yao ili wasiambukizwe 

Pia  Nchimbi  alitoa wito kwa  taasisi  na mashirika  yanayotoa huduma  za upimaji wa  virusi vya ukimwi kwa  wananchi  kuongeza  mikakati ya  kuwataka  wananchi  waweze  kujitokeza  kwa wingi  kupima virusi vya ukimwi  kwa hiari yao.

Jairy  Khanga mganga  mkuu  wa  Mkoa wa Ruvuma  katika taarifa yake  ailidai mkoa  wa Ruvuma  unavituo vya  kutolea huduma  za afya 348 ambapo  vituo  295 sawa na asilimia  85 vinatoa  huduma  ya unasihi  na upimaji ,289 sawa na asilimia 83 vinatoa  huduma ya kuzuia maambukizi  ya VVU kutoka  kwa mama wajawazito  na wanaonyonyesha  kwenda  kwa  mtoto.vituo 165 sawa na asilimia 47 vinatoa  huduma ya tiba na matunzo  ya watu  wanaoishi  na virusi vya ukumwi , vituo 41 sawa na asilimia 12 vinatoa  huduma za tiba kinga vya virusi vya ukimwi kabla ya kudhurika  na vituo 30 sawa na asilimia 9 vinatoa huduma  za tohara kwa wanaume.

Hata hivyo bwana  Khanga  alisema mkoa  wa Ruvuma  upo  juu  kimaambukizi  zaidi ya kiwango  cha taifa  cha maambukizi  kwa asilimia  0.9 kadiri ya matokeo ya  utafiti  wa kiashiria  cha UKIMWI  Tanzania wa mwaka  2016mpaka 2017.

Bwana Khanga alisema  licha  ya  kiwango cha maambukizi  kimkoa kuwa  asilimia 5.6  na kukizidi   kiwango cha maambukizi  kitaifa  ambacho ni  asilimia  4.7  mkoa huo umepunguza  ongezeko la maambukizi  kutoka  asilimia 7 mwaka  2011-2012 mpaka kufikia asilimia  5.6 sawa  na asilimia 1.4 hivi sasa.

Mohamedi  Ally Geho  katibu wa baraza  la watu wanaoishi na virusi vya ukimwi katika wilaya ya Namtumbo  aliwataka wananchi wenzake kujitokeza kupima  virusi  vya  ukimwi na kupata huduma za afya  ili kuishi kwa matumaini kwa kuwa yeye  anaendelea kuishi  na sasa  anazaidi ya miaka  16 tangu agundulike  anavirusi vya  ukimwi

Naye  Rabia Miraji Gunda  kutoka kijiji cha Suruti  aliwaambia wananchi katika maadhimisho hayo  kuwa  yeye  aligundulika na virusi vya ukimwi wakati  wa ujauzito wake  na hivyo  amejifungua  mtoto  na kupatiwa huduma za  kiafya  yeye  pamoja na mtoto  wake  hali zao zinaridhisha na hawana  wasiwasi wowote.

Maadhimisho  ya siku ya ukimwi duniani  huadhimishwa kila mwaka ifikapo tarehe  1mwezi Desema  ambapo  kwa mwaka huu 2020 kauli mbiu  ya  Maadhimisho hayo  ilikuwa “Ushirikiano  wa Kimataifa ,Uwajibikaji  wa  pamoja”

MWISHO.

Matangazo

  • Orodha ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka 2021 kutoka katika shule mbalimbali za msingi za Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma December 18, 2020
  • Kimolo Secondary School Joining instruction December 18, 2020
  • Korido Secondary School Joining Instruction December 18, 2020
  • Lisimonji Secondary School Joining Instruction December 18, 2020
  • Ona zote

Habari Mpya

  • MJUMITA watoa mafunzo ya utawala bora namtumbo

    January 19, 2021
  • DC namtumbo awataka askari wa akiba kuilinda amani.

    January 19, 2021
  • mbunge namtumbo aupongeza uongozi sonamcu

    January 18, 2021
  • atamani namtumbo kuwa na timu ligi kuu

    January 03, 2021
  • Ona zote

Video

HOTUBA YA WAZIRI WA TAMISEMI
Video

Kurasa za Haraka

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Halmashauri ya Songea
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Nyasa
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru

Tovuti Mashuhuri

  • TAMISEMI
  • Ikulu ya Tanzania
  • Tume ya Utumishi wa Umma
  • Baraza la Mitihani
  • Tume ya ajira Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo

    Anuani: S.L.P 55 NAMTUMBO

    Simu ya Mezani: 0252675008

    Simu ya Mkononi: 0765142640

    Barua Pepe: ded@namtumbodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki©2018Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo. Haki zote Zimehifadhiwa.