• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Complaints |
    • Gms |
Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu ya Halmashauri
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji/Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi, Maliasili na Utalii
      • Mipango, Uchumi na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Utumishi na Utawala
      • Maji
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi na Zimamoto
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA)
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • TASAF
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Fursa za Kilimo
    • Fursa za ufugaji
    • Fursa za Madini
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Huduma za Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Mheshimiwa Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokalika
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma/Vyombo Mbalimbali vya Habari
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali

Diwani awataka viongozi wa Serikali kujitokeza katika migogoro ya binadamu na wanyamapori

Tarehe ya Kuweka: April 16th, 2024

DIWANI AWATAKA VIONGOZI WA SERIKALI  KUWAJENGA WANANCHI KISAIKOLOJIA  MIGOGORO YA WANYAMAPORI NA BINADAMU

Diwani wa kata ya Likuyu Wilayani Namtumbo Mkoani Ruvuma Kassimu Gunda aliwataka viongozi wa Serikali Kuwajenga wananchi kisaikolojia hasa kwenye migogoro kati ya binadamu na wanyamapori.


Gunda alisema ipo Tabia ya viongozi kutojitokeza kwenye migogoro kati ya wanyamapori na binadamu hasa linapotokea binadamu kuuawa na Tembo Kwa kuogopa Wananchi kuwa na hasira Kwa viongozi wao badala ya viongozi kuungana na wananchi Kuwajenga kisaikolojia ili wajue viongozi wao nao wanaumia na matatizo wanayowapata wananchi wao.


Gunda alifafanua faida ya viongozi kuwa na wananchi wakati wa matatizo Yao unawajenga wananchi kisaikolojia kuwa  unajali matatizo Yao Kwa kushirikiana nao bega Kwa bega .


Hata hivyo Gunda alidai uwepo wa viongozi wakubwa katika migogoro ya wananchi wanakuwa na Imani na viongozi wao pale wanapoona wanajitokeza katika shida zao na kuwapa pole na faraja .


Pamoja na hayo yote Gunda aliiomba serikali Kuharakisha kifutajasho ili wananchi walioathirika na uharibifu wa mazao Yao na  wanyamapori waweze Kununua chakula ambacho kiliharibiwa na wanyamapori hao.


Menas Fusi mkazi wa kitongoji Cha mfuate Kijiji Cha Likuyu alisema kasi ya wanyama Tembo Kuja katika mashamba ya wakulima imepungua Kutokana  na kuwepo Kwa Jeshi la TANAPA ambalo Kwa kiasi kikubwa hufanya kazi ya kuwarudisha Tembo hao katika hifadhi .


Fusi alisema Tembo mmoja mwenye mtoto alimsababishia kifo  Merania Lukas Magazini (62) mkazi wa Kijiji Cha Likuyu aliyekuwa amejihimu shambani na alipofika maeneo ya msituni akakutana na Tembo huyo na kumsababishia kifo.


Hata hivyo Fusi aliiomba serikali kufanya utafiti wa Tembo waliovuka mipaka Yao Kwa kuwa sio wengi wawarudishe kwenye hifadhi ya wanyama badala ya kuwaacha katika misitu ya vijiji .


Afisa Maliasili na Utalii wa Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo priska Msuha alisema Licha ya kutokea Changamoto ya Tembo mmoja mwenye mtoto kumua mwananchi katika Kijiji Cha Likuyu Changamoto ya Tembo imepungua Kutokana na Kambi ya TANAPA kufanya kazi kubwa ya kuwarudisha wanyamapori hao hifadhini lakini pia wananchi Kujua madhara na namna ya kukabiliana na Tembo wanapoingia katika makazi ya watu.


Priska alisema huko Nyuma kabla ya kutolewa elimu ya namna yakufanya wakimwona mnyama Tembo ,wananchi waliokuwa wakimwona Tembo katika makazi yao waliokuwa wanapiga kelele na kumfuata lakini Kwa Sasa wananchi wakimwona Tembo hawamfuati hubaki kimya  hupiga simu ili mamlaka zinazohusika hufika haraka na kuwaondoa Tembo hao katika makazi ya watu.


Hata hivyo watumishi wa idara ya Maliasili na Utalii Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo wametawanywa katika maeneo yenye Changamoto ya Tembo kuingia katika makazi ya watu ili kushirikiana na askari wasaidiazi wa wanyapori wa vijiji katika kukabiliana na Changamoto zitakazojitokeza kutoka Kwa wanyama hao.

Mwisho.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA 2025 KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA NAMTUMBO January 18, 2025
  • MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI KATIKA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA NAMTUMBO MWAKA 2025 January 12, 2025
  • Ona zote

Habari Mpya

  • DC NGOLLO MALENYA AWAFARIJI WAHANGA WA RADI KATIKA KATA YA LUSEWA WILAYA YA NAMTUMBO

    February 21, 2025
  • WANANCHI NAMTUMBO WAMSHUKURU RAIS SAMIA

    January 06, 2025
  • MATREKTA aliyogawa Rais Samia yawanufaisha wananchi wa Wilaya ya Namtumbo, katika kuongeza Uzalishaji kwenye kilimo cha Kisiasa.

    January 06, 2025
  • Sukrani kwa Mhe.Rais wa wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan

    January 05, 2025
  • Ona zote

Video

HOTUBA YA WAZIRI WA TAMISEMI
Video

Kurasa za Haraka

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Halmashauri ya Songea
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Nyasa
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru

Tovuti Mashuhuri

  • TAMISEMI
  • Ikulu ya Tanzania
  • Tume ya Utumishi wa Umma
  • Baraza la Mitihani
  • Tume ya ajira Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo

    Anuani: 2 Barabara ya Boma, S.L.P 55, 57382 NAMTUMBO

    Simu ya Mezani: 0252675008

    Simu ya Mkononi: 0767519181

    Barua Pepe: ded@namtumbodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki©2021Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo. Haki zote Zimehifadhiwa.