• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Complaints |
    • Gms |
Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu ya Halmashauri
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji/Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi, Maliasili na Utalii
      • Mipango, Uchumi na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Utumishi na Utawala
      • Maji
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi na Zimamoto
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA)
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • TASAF
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Fursa za Kilimo
    • Fursa za ufugaji
    • Fursa za Madini
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Huduma za Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Mheshimiwa Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokalika
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma/Vyombo Mbalimbali vya Habari
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali

Madiwani Namtumbo Kuwasilisha Mapendekezo Kufuta hifadhi za vijiji (WMA's)

Tarehe ya Kuweka: November 21st, 2023

MADIWANI NAMTUMBO KUWASILISHA  MAPENDEKEZAO KUFUTA HIFADHI




Wakiongea kwenye vikao vya  kamati na kikao kazi madiwani wa Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo walipendekeza kufutwa Kwa hifadhi za jamii za vijiji katika Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo.



Mwenyekiti wa kamati ya uchumi ,ujenzi na Mazingira Charles Chengula alisema malalamiko ya waheshimiwa madiwani ,wananchi wa wilaya ya Namtumbo kuhusu kutenga maeneo ya hifadhi za jumuiya ya Mbarang'andu,Kimbanda na kisungule yalikuwa mazuri Kwa wananchi wa jumuiya hizo lakini Jumuiya hizo zimevamiwa na wafugaji na kuharibu Mazingira ya uhifadhi huo.


Chengula alidai wakulima waliokuwa wanalima katika maeneo ya hifadhi waliondolewa Kwa nguvu na wengine kufikishwa mahakamani na kufungwa Kwa Mujibu wa Sheria lakini wafugaji wapo katika maeneo hayo hayo na kuendesha shughuli zao za kilimo kufuga na kuchunga katika maeneo ambayo wakulima waliondolewa Kupisha uhifadhi.


Hata hivyo Chengula pamoja na mambo mengine alisema malalamiko ya kuwaondoa wakulima katika maeneo ya hifadhi Kwa nguvu huku wafugaji wakiendesha shughuli zao katika maeneo hayo hayo yanawapa wakati mgumu waheshimiwa madiwani kujibu maswali hayo kutoka Kwa wananchi.


Mheshimiwa Chengula aliwataka wajumbe kufikia uamuzi juu ya tatizo Hilo Kwa kuwa Halmashauri kupitia ofisi ya Mkurugenzi  wamelalamikia Sana swala la wafugaji kufanya shughuli zao katika maeneo ya hifadhi lakini wafugaji hao wanaishi huko Kwa nguvu na wataalamu wa Halmashauri wanapotaka kufanya kazi ya kuwahamisha wafugaji huwapiga wataalamu hao Kwa kuwajeruhi na mapanga pamoja na mikuki


Bakiri Mawila diwani wa kata ya Lisimonji wilayani humo alidai kuendelea kuwa na hifadhi za vijiji (WMA's) ni kujidanganya Kwa kuwa hifadhi hizo zimevamiwa na wafugaji Kwa kulima ,kuchunga mifugo pamoja na kukata miti Hali inayoondoa hadhi ya uhifadhi huo


Mawila alifafanua kuwa kitendo Cha wafugaji kubaki katika hifadhi huku wakiharibu Mazingira ya uhifadhi ni heri Sasa tupendekeze kuondoa uhifadhi huo Ili maeneo hayo yatumiwe na wananchi katika shughuli za kilimo badala ya kuwaacha wafugaji pekee wakiharibu Mazingira ya hifadhi huku wananchi wengine wakilalamikia kuondolewa katika maeneo hayo kupisha hifadhi.


Salumu Kabumaye Diwani wa kata ya Mchomoro alidai muda wa kupendekeza kufutwa Kwa hifadhi hizo umefika ili kuondoa malalamiko ya wananchi kuwa tunawaoneo wakulima na kuwapendelea wafugaji Kwa kuwaondoa wakulima katika hifadhi na kuwaacha wafugaji katika hifadhi.


Gervas Mwalyombo afisa misitu wa Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo alisema nguvu za ziada zinahitajika kuwaondoa wafugaji waliovamia katika maeneo ya misitu ya hifadhi lakini Kwa kuwategemea watumishi wa idara ya misitu na wanyamapori  pekee hawataweza kwani huhatarisha maisha Yao Kwa kupigwa na mikuki na mishale kutoka Kwa wafugaji hao alisema Mwalyombo.


Mapendekezo ya kufutwa Kwa hifadhi hizo yanatarajiwa kufikishwa katika baraza la madiwani Ili yapitishwe na waheshimiwa madiwani  katika kikao Cha baraza la madiwani linalotarajiwa kufanyika hivi karibuni.

Mwisho.



Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA 2025 KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA NAMTUMBO January 18, 2025
  • MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI KATIKA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA NAMTUMBO MWAKA 2025 January 12, 2025
  • Ona zote

Habari Mpya

  • DC NGOLLO MALENYA AWAFARIJI WAHANGA WA RADI KATIKA KATA YA LUSEWA WILAYA YA NAMTUMBO

    February 21, 2025
  • WANANCHI NAMTUMBO WAMSHUKURU RAIS SAMIA

    January 06, 2025
  • MATREKTA aliyogawa Rais Samia yawanufaisha wananchi wa Wilaya ya Namtumbo, katika kuongeza Uzalishaji kwenye kilimo cha Kisiasa.

    January 06, 2025
  • Sukrani kwa Mhe.Rais wa wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan

    January 05, 2025
  • Ona zote

Video

HOTUBA YA WAZIRI WA TAMISEMI
Video

Kurasa za Haraka

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Halmashauri ya Songea
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Nyasa
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru

Tovuti Mashuhuri

  • TAMISEMI
  • Ikulu ya Tanzania
  • Tume ya Utumishi wa Umma
  • Baraza la Mitihani
  • Tume ya ajira Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo

    Anuani: 2 Barabara ya Boma, S.L.P 55, 57382 NAMTUMBO

    Simu ya Mezani: 0252675008

    Simu ya Mkononi: 0767519181

    Barua Pepe: ded@namtumbodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki©2021Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo. Haki zote Zimehifadhiwa.