• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Complaints |
    • Gms |
Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu ya Halmashauri
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji/Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi, Maliasili na Utalii
      • Mipango, Uchumi na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Utumishi na Utawala
      • Maji
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi na Zimamoto
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA)
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • TASAF
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Fursa za Kilimo
    • Fursa za ufugaji
    • Fursa za Madini
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Huduma za Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Mheshimiwa Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokalika
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma/Vyombo Mbalimbali vya Habari
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali

Mbunge Namtumbo akabidhi mifuko 30 ya simenti na madawati 40

Tarehe ya Kuweka: October 16th, 2023

Mbunge Namtumbo akabidhi  mifuko ya smenti 40 na madawati 30.


Mbunge wa Jimbo la Namtumbo Mkoani Ruvuma Vitta Rashid Kawawa amekabidhi mifuko ya simenti 40 na madawati 30 katika shule ya msingi Upendo .


Akikabidhi mifuko hiyo pamoja na madawati Kawawa alisema anatimiza ahadi yake aliyohaidi katika ziara yake ya tarehe 16.9.2023 alipotembelea Kijiji Cha Mputa na wananchi kumwomba msaada wa kuisaidia shule ya  msingi upendo


Aidha Kawawa aliwashukuru wananchi wa Kijiji Cha Mputa Kwa ushirikiano wao wa kujenga shule  ya msingi Upendo lakini akadai Ofisi ya Mbunge itahakikisha shule hiyo inapata fedha kama shule zingine .


Hata hivyo Kawawa alimwagiza Afisa elimu vifaa na takwimu aliyemwakilisha afisa elimu msingi katika makabidhiano hayo kuwa ofisi ya elimu msingi inatakiwa kutenga bajeti ya kujenga madarasa ,Nyumba za walimu na vyoo Kwa ajili ya shule hiyo


Pamoja na hayo Kawawa aliiagiza idara ya elimu kuwa ushiriki wao katika miradi ijayo ya boost Namtumbo wahakikishe shule ya msingi Upendo inapewa kipaumbele katika bajeti ya boost Ili kuondoa changamoto

Afisa elimu vifaa na takwimu Lulu Mapunda alimshukuru mbunge wa Jimbo la Namtumbo Vitta Rashid Kawawa Kwa kuisaidia shule hiyo madawati 30 na mifuko ya simenti mifuko 40 Ili kuisaidia shule hiyo kuboresha miundombinu yake.


Afisa elimu ,Elimu ya watu wazima Shaibu Majiwa pamoja na kumpongeza Mbunge wa Jimbo la Namtumbo Vitta Rashid Kawawa Kwa upendo wake wa kusaidia huduma za jamii aliwaambia wananchi wa Kijiji Cha Mputa kuwa mbunge huyo ni mnyenyekevu,mpole na msikivu Kwa wananchi wake .


Majiwa alifafanua kuwa unyenyekevu wake akiwa bungeni humsaidia kuomba fedha za miradi na kuifanya Namtumbo kuwa na miradi mingi yenye fedha nyingi alisema Majiwa.


Shakimu Sudi Ngonyani akiongea Kwa niaba ya wazee wa Kijiji Cha Mputa alisema wazee wa Kijiji Cha Mputa wanamshukuru mbunge Kawawa Kwa jitihada yake ya kuisaidia shule hiyo pamoja na wananchi wa Jimbo la Namtumbo .


Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Upendo Laika Hassan Ngonyani pamoja na kumshukuru Mh.Mbunge wa Namtumbo Vitta Kawawa Kwa msaada wake wa smenti mifuko 40 na madawati 30 aliendelea kumwomba mbunge huyo kuwa shule hiyo Bado inachangamoto ya  Nyumba za walimu ,madarasa yenye sakafu ya vumbi huku akidai wananchi wamejenga  Nyumba moja ya mwalimu Kwa nguvu zao na imeishia hatua ya linta ambapo Mbunge wa Jimbo Hilo akakubali  Kutoa milioni tano(5,000,000) Kwa ajili  ya kuweka ringbeam ya Nyumba ya mwalimu pamoja na kuezeka..


Shule ya msingi Upendo ilianzishwa Kwa nguvu za wananchi mwaka 2007 yenye jumla ya madarasa Saba ,ikiwa na idadi ya wanafunzi 352 ikiwa na wanafunzi wavulana 158 na wasichana 194 huku kukiwa na jumla ya walimu watano ikiwa wakike 2 na wakiume 3 .


Shule ya msingi Upendo IPO katika Kijiji Cha Mputa kata ya Mputa na kitendo Cha mbunge Kutoa madawati  yenye thamani ya shilingi 1,650,000 na mifuko ya smenti yenye  thamani ya shilingi 700,000 katika shule hiyo imesaidia kupunguza changamoto zilizopo katika shule hiyo.

Mwisho.














Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA 2025 KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA NAMTUMBO January 18, 2025
  • MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI KATIKA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA NAMTUMBO MWAKA 2025 January 12, 2025
  • Ona zote

Habari Mpya

  • DC NGOLLO MALENYA AWAFARIJI WAHANGA WA RADI KATIKA KATA YA LUSEWA WILAYA YA NAMTUMBO

    February 21, 2025
  • WANANCHI NAMTUMBO WAMSHUKURU RAIS SAMIA

    January 06, 2025
  • MATREKTA aliyogawa Rais Samia yawanufaisha wananchi wa Wilaya ya Namtumbo, katika kuongeza Uzalishaji kwenye kilimo cha Kisiasa.

    January 06, 2025
  • Sukrani kwa Mhe.Rais wa wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan

    January 05, 2025
  • Ona zote

Video

HOTUBA YA WAZIRI WA TAMISEMI
Video

Kurasa za Haraka

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Halmashauri ya Songea
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Nyasa
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru

Tovuti Mashuhuri

  • TAMISEMI
  • Ikulu ya Tanzania
  • Tume ya Utumishi wa Umma
  • Baraza la Mitihani
  • Tume ya ajira Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo

    Anuani: 2 Barabara ya Boma, S.L.P 55, 57382 NAMTUMBO

    Simu ya Mezani: 0252675008

    Simu ya Mkononi: 0767519181

    Barua Pepe: ded@namtumbodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki©2021Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo. Haki zote Zimehifadhiwa.