• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Complaints |
    • Gms |
Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu ya Halmashauri
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji/Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi, Maliasili na Utalii
      • Mipango, Uchumi na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Utumishi na Utawala
      • Maji
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi na Zimamoto
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA)
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • TASAF
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Fursa za Kilimo
    • Fursa za ufugaji
    • Fursa za Madini
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Huduma za Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Mheshimiwa Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokalika
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma/Vyombo Mbalimbali vya Habari
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali

MKOA WA RUVUMA WACHANGIA ASILIMIA 3.8 YA PATO LA TAIFA

Tarehe ya Kuweka: January 1st, 2023

MKOA WA RUVUMA WACHANGIA ASILIMIA 3.8 YA PATO LA TAIFA

UCHUMI wa Mkoa wa Ruvuma umeendelea kuimarika kwa kuchangia asilimia 3.8 ya pato la Taifa ukiwa juu ya mikoa mingine ya Kanda ya Kusini Mashariki.

Kwa mujibu wa Takwimu kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu,uchumi wa Mkoa wa Ruvuma umeendelea kuimarika ambapo Pato la Taifa (GDP) kwa bei za mwaka husika,pato la Mkoa liliendelea kuongezeka kutoka shilingi bilioni 3.147 mwaka 2014 hadi kufikia shilingi bilioni 6.106 mwaka 2021.

Mchumi Mkuu kutoka Benki Kuu ya Tanzania(BOT) Kanda ya Mtwara Peter Stanlaus akizungumzia hali ya uchumi wa Mkoa wa Ruvuma kwenye kikao cha Baraza la Ushauri la Mkoa wa Ruvuma(RCC) amelitaja wastani la pato kwa mtu (GDP per capital) katika Mkoa limeendelea kuongezeka na kuwa juu ya wastani wa pato la mtu kitaifa.

“Wastani wa pato kwa mtu kwa mwaka katika Mkoa wa Ruvuma liliongezeka kutoka shilingi 2,184,532 mwaka 2014 hadi kufikia shilingi  3,602,162 mwaka 2021 ikilinganishwa na wastani wa pato kwa mtu kitaifa la shilingi 2,798,244 kwa mwaka’’,alisema.

Hata hivyo Mchumi Mkuu huyo wa BOT amesema hali ya mfumko wa bei katika Mkoa wa Ruvuma katika kipindi cha mwaka 2021/2022 ulibakia kwenye wastani wa asilimia 3.2 kutokana na kuimarika kwa ugavi wa chakula na kuongezeka kwa uzalishaji wa chakula.

Akizungumzia  Mkoa wa Ruvuma ulivyochangia uchumi kupitia sekta ya madini,Mchumi Mkuu huyo wa BOT amesema sekta ya madini imeendelea kuimarika katika Kanda ya Kusini Mashariki ambapo kwa mwaka 2021/2022 ilichangia shilingi bilioni 728.9.

Hata hivyo ameutaja Mkoa wa Ruvuma kuwa katika sekta ya madini kwenye Kanda hiyo,ulichangia asilimia 69.9 ya thamani ya mapato yote ambapo uchimbaji wa madini ya makaa ya mawe kutoka Ruvuma pekee umechangia asilimia 96.4 ya thamani ya madini yote kanda ya Kusini Mashariki.

Akizungumza baada ya kupokea taarifa hiyo ya BOT,Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas amewapongeza wananchi wote wa Mkoa wa Ruvuma hasa kwenye sekta za kilimo na madini  walivyoshiriki kikamilifu kuimarisha uchumi wa Mkoa.

“Kabla ya ripoti hii nilidhani naongoza Mkoa masikini,kumbe Mkoa wa Ruvuma ni Mkoa tajiri kwa sababu pato la mtu lipo juu ya wastani wa pato la mtu kitaifa’’.alisisitiza RC Thomas.

Mkoa wa Ruvuma umeendelea kuwa kapu la chakula la Taifa kwa kuongoza mfululizo kitaifa kwa miaka minne katika uzalishaji wa chakula nchini.

Yeremias Ngerangera

Namtumbo

Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA YA WAOMBAJI WA KAZI YA MUDA YA SENSA WALIOFAULU USAILI NA KUITWA KWENYE MAFUNZO July 27, 2022
  • TAARIFA KWA UMMA June 27, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WAOMBAJI WA KAZI YA MUDA YA SENSA WALIOFAULU USAILI NA KUITWA KWENYE MAFUNZO July 27, 2022
  • MABADILIKO YA TAREHE YA KUFANYA USAILI June 22, 2022
  • Ona zote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NAMTUMBO LAPITISHA MAPENDEKEZO YA MPANGO WA BAJETI 2023/2024

    January 30, 2023
  • MAADHIMISHO YA KUZALIWA KWA RAIS SAMIA YAAMBATANA NA UPANDAJI WA MITI RUVUMA

    January 27, 2023
  • SHULE 16 NAMTUMBO ZANUFAIKA NA WALIMU WA MAZOEZI YA KUFUNDISHA

    January 26, 2023
  • MIFUGO MINGINE 508 YAKAMATWA NAMTUMBO

    January 25, 2023
  • Ona zote

Video

HOTUBA YA WAZIRI WA TAMISEMI
Video

Kurasa za Haraka

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Halmashauri ya Songea
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Nyasa
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru

Tovuti Mashuhuri

  • TAMISEMI
  • Ikulu ya Tanzania
  • Tume ya Utumishi wa Umma
  • Baraza la Mitihani
  • Tume ya ajira Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo

    Anuani: S.L.P 55 NAMTUMBO

    Simu ya Mezani: 0252675008

    Simu ya Mkononi: 0765142640

    Barua Pepe: ded@namtumbodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki©2021Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo. Haki zote Zimehifadhiwa.