• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Complaints |
    • Gms |
Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu ya Halmashauri
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji/Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi, Maliasili na Utalii
      • Mipango, Uchumi na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Utumishi na Utawala
      • Maji
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi na Zimamoto
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA)
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • TASAF
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Fursa za Kilimo
    • Fursa za ufugaji
    • Fursa za Madini
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Huduma za Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Mheshimiwa Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokalika
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma/Vyombo Mbalimbali vya Habari
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali

NAMTUMBO KUMWAGIWA MABILIONI FEDHA ZA MRADI HEWA UKAA

Tarehe ya Kuweka: March 29th, 2022

Akitoa taarifa  ya mradi  wa hewa ukaa katika mafunzo ya kuwajengea uwezo na uelewa waheshimiwa madiwani ,wadau wa maendeleo na wakuu wa idara na vitengo wa halmashauri ya wilaya ya Namtumbo afisa wanyama pori na misitu wa halmashauri ya wilaya hiyo Prisca Msuha alisema mradi wa hewa ukaa utaifanya Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo kumwagiwa mabilioni ya fedha wakati mradi utakapoanza kazi.

Priska katika taarifa yake alidai mradi wa hewa ukaa utatekelezwa katika vijiji vinavyopatikana katika jumuiya za  uhifadhi za  wanyamapori za kimbanda,kisungule na Mbarangā€andu zilizopo katika kata za Kitanda,Mgombasi,Ligera,Msisima,Mchomoro,Magazini,Lusewa na Likuyuseka.

Priska alisisitiza idara yake kwa kushirikiana na wadau wa uhifadhi TAWA,TANAPA,na TFS  walishatoa mafunzo kwa viongozi wa vijiji, watendaji wa vijiji ,kata na wadau mbalimbali wa maendeleo katika ngazi ya kata na vijiji kuhusu mpango wa hewa ukaa .

Aidha Priska alifafanua lengo la  mpango wa hewa ukaa ni kuzinufaisha jamii inayotunza misitu ambayo hewa yake kutoka katika misitu hiyo ndiyo inayosaidia kunyonya hewa chafu inayozalishwa katika viwanda vikubwa duniani ili waendelee kulinda na kupanda miti katika mazingira yao .

Diwani wa kata ya Likuyuseka Kassim Gunda alisisitiza kuwepo kwa uwazi katika kutekeleza mpango huo na kuagiza idara inayohusika kushirikisha jamii moja kwa moja ili kuepuka sintofahamu ambayo inaweza kutokea kama jamii ambayo ndiyo yenye maeneo ya uhifadhi kutofahamu vizuri juu ya mpango huo.

Diwani  huyo alidai ushirikishwaji wa jamii katika kutekeleza mpango huo upewe kipaumbele kwani jamii  ndio inayotakiwa kupatiwa elimu zaidi kutokana na maeneo ya uhifadhi hayo yapo katika vijiji ambapo jamii hiyo ndiyo ipo ili kuepusha migogoro ambayo inaweza kujitokeza hapo baadae alisema diwani huyo.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo Jumma Pandu aliwasisitizia waheshimiwa madiwani kwenda kuelimisha jamii katika maeneo yanayoenda kutekeleza mradi huo kuelimisha jamii umuhimu wa mradi huo kwa jamii,halmashauri na serikali kwa ujumla.

Pandu aliwataka madiwani kwenda kuwaelekeza wananchi matumizi ya maeneo na kuzingatia kutochanganya matumizi ya maeneo na kwenda kuwasisitizia wananchi kutumia maeneo kama yalivyopangwa katika mpango wa matumizi bora ya ardhi yao.

Nchini Tanzania mradi wa hewa ukaa unatekelezwa katika wilaya za Kiteto,Tanganyika ,karatu na Makame  ambapo kwa wilaya ya Tanganyika yenye lenye eneo la msitu wa kilomita 2500 hunufaika na shilingi 3,000,000,000 kwa mwaka.

Mwisho.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA 2025 KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA NAMTUMBO January 18, 2025
  • MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI KATIKA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA NAMTUMBO MWAKA 2025 January 12, 2025
  • Ona zote

Habari Mpya

  • DC NGOLLO MALENYA AWAFARIJI WAHANGA WA RADI KATIKA KATA YA LUSEWA WILAYA YA NAMTUMBO

    February 21, 2025
  • WANANCHI NAMTUMBO WAMSHUKURU RAIS SAMIA

    January 06, 2025
  • MATREKTA aliyogawa Rais Samia yawanufaisha wananchi wa Wilaya ya Namtumbo, katika kuongeza Uzalishaji kwenye kilimo cha Kisiasa.

    January 06, 2025
  • Sukrani kwa Mhe.Rais wa wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan

    January 05, 2025
  • Ona zote

Video

HOTUBA YA WAZIRI WA TAMISEMI
Video

Kurasa za Haraka

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Halmashauri ya Songea
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Nyasa
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru

Tovuti Mashuhuri

  • TAMISEMI
  • Ikulu ya Tanzania
  • Tume ya Utumishi wa Umma
  • Baraza la Mitihani
  • Tume ya ajira Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo

    Anuani: 2 Barabara ya Boma, S.L.P 55, 57382 NAMTUMBO

    Simu ya Mezani: 0252675008

    Simu ya Mkononi: 0767519181

    Barua Pepe: ded@namtumbodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki©2021Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo. Haki zote Zimehifadhiwa.