• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Complaints |
    • Gms |
Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu ya Halmashauri
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji/Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi, Maliasili na Utalii
      • Mipango, Uchumi na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Utumishi na Utawala
      • Maji
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi na Zimamoto
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA)
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • TASAF
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Fursa za Kilimo
    • Fursa za ufugaji
    • Fursa za Madini
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Huduma za Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Mheshimiwa Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokalika
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma/Vyombo Mbalimbali vya Habari
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali

Wananchi Namtumbo walalamikia kuchelewa kuchimba madini ya Urani

Tarehe ya Kuweka: August 3rd, 2023

WANANCHI NAMTUMBO WALALAMIKIA KUCHELEWA UCHIMBAJI MADINI YA URANI.

Wananchi wa mamlaka ya mji mdogo wa Namtumbo Mkoani Ruvuma wamelalamikia kuchelewa kuanza Kwa mradi wa uchimbaji wa madini ya Urani.


Wakizungumza kwenye mkutano wa hadhara na mbunge wa Jimbo la Namtumbo Vitta Rashid Kawawa ,walisema tunashangaa kuona mradi wa uchimbaji wa madini ya Urani umebaki kimya licha ya kupewa matumaini ya kuanza Kwa mradi huo.


Shami Kingovaye mwananchi wa kata ya Rwinga mamlaka ya mji mdogo wa Namtumbo alihoji ukimya wa kuanza Kwa uchimbaji wa madini ya Urani katika Kijiji Cha Likuyuseka wilayani Namtumbo.


Kingovaye alidai wananchi wa Namtumbo walikuwa na matumaini makubwa ya kuanza Kwa mradi huo kutawanufaisha wananchi kiuchumi Kwa kuuza bidhaa zao kupitia mkusanyiko wa watu watakaokuwepo wakati wa uchimbaji wa madini huo.


Pia Kingovaye alisema wananchi wa Namtumbo walitegemea kupata ajira mbalimbali kutokana na kuanza Kwa mradi huo lakini wanashangaa ukimya wa kuanza Kwa mradi huo.


Rashid Nihuka Kwa upande wake alihoji Kuna maana Gani ya kuanzisha stendi ya wilaya wakati magari ya vijijini yanapitiliza na kuelekea Songea na wananchi kuendelea kununua bidhaa songea na kuziacha bidhaa za hapa Namtumbo.


Nihuka alihoji wakati wa barabara ya vumbi kabla ya kuwekwa lami nauli ya Namtumbo mpaka Songea ilikuwa shilingi 2500 mpaka 2000 ilikuwa unafika songea lakini baada ya kuwekwa lami nauli zimepanda mpaka 4000 mpaka 3500 alisema Nihuka.


Mbunge wa Namtumbo Vitta Kawawa pamoja na kuwashukuru wananchi wa kata ya Rwinga kutumia muda wao na kuhudhuria mkutano wake Ili waweze kuelezea kero zao.


Kawawa aliwaeleza wananchi wa kata ya Rwinga kuwa haijawahi kutokea katika awamu zote za Marais Namtumbo kupata miradi kama ilivyopata safari hii ya Dkt Samia Suluhu Hassan .


Akijibu kero ya kuchelewa kuchimba madini ya Urani Kawawa alisema Kuna changamoto iliyojitokeza kati ya TANAPA na kampuni iliyopewa jukumu la kuchimba madini hayo.


Kampuni ya Mantra iliyopewa jukumu la kuchimba madini hayo ilikumbana na kikwazo hicho na kusubiria utaratibu mwingine unaofanywa na Serikali alisema mbunge huyo.


Aidha Kawawa alifafanua kuwa awali changamoto ilikuwa eneo linalotakiwa kuchimba madini hayo lipo katika hifadhi na eneo ambalo ni urithi wa Dunia( world heritage) na kulingana na Sheria za kimataifa za uhifadhi hazitakiwa kufanyika shughuli yoyote ya kibinadamu bila idhini ya mamlaka husika.


 Kawawa aliwaambia mwananchi kuwa Serikali ililiondoa eneo Hilo kwenye hifadhi Ili kuiwezesha kampuni ya Mantra iliyopewa idhini ya kuchimba madini hayo iweze kuchimba ,hata hivyo kampuni hiyo haikuweza kuanza mradi wa kuchimba madini hayo baada ya kushuka bei katika soko la Dunia.


Wakati kampuni hiyo ikisubiri bei nzuri katika soko la Dunia eneo Hilo la hifadhi ambapo Serikali iliamua kulitoa kwenye hifadhi kutoka hifadhi ya taifa ya selou Kwa wakati ule na kukitenga kipande Cha eneo kilichokuwa na madini ya Urani na kukipa jina la Undendeule forest Ili kuruhusu madini hayo yaweze kuchimbwa Kwa manufaa makubwa ya taifa lakini baada ya hifadhi kuitwa hifadhi ya taifa ya Nyerere na kuwa chini ya TANAPA na Kwa Mujibu wa mbunge alisema imejitokeza changamoto Tena kwa TANAPA kuhusu kutokuwa na taarifa ya uchimbaji huo wa madini katika maeneo ambayo yapo chini Yao lakini Serikali inalifanyia kazi alisema Kawawa.


Kuhusu nauli za mabasi mheshimiwa Kawawa aliwataka wananchi kuwa na subira atalifuatilia jambo Hilo kwenye mamlaka husika na kuhusu stendi ya wilaya alisema atalipeleka kwenye vikao vya kisheria vya maamuzi vya wilaya Ili likajadiliwe na kupatiwa majawabu yake.


Mbunge wa Namtumbo Vita Kawawa anaendelea na ziara yake ya kuzungumza na wananchi kupitia mikutano ya hadhara Kwa kusikiliza kero na kuzipatia majawabu Kwa kushirikana na wakuu wa idara wa Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo

Mwisho.



Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA 2025 KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA NAMTUMBO January 18, 2025
  • MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI KATIKA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA NAMTUMBO MWAKA 2025 January 12, 2025
  • Ona zote

Habari Mpya

  • DC NGOLLO MALENYA AWAFARIJI WAHANGA WA RADI KATIKA KATA YA LUSEWA WILAYA YA NAMTUMBO

    February 21, 2025
  • WANANCHI NAMTUMBO WAMSHUKURU RAIS SAMIA

    January 06, 2025
  • MATREKTA aliyogawa Rais Samia yawanufaisha wananchi wa Wilaya ya Namtumbo, katika kuongeza Uzalishaji kwenye kilimo cha Kisiasa.

    January 06, 2025
  • Sukrani kwa Mhe.Rais wa wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan

    January 05, 2025
  • Ona zote

Video

HOTUBA YA WAZIRI WA TAMISEMI
Video

Kurasa za Haraka

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Halmashauri ya Songea
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Nyasa
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru

Tovuti Mashuhuri

  • TAMISEMI
  • Ikulu ya Tanzania
  • Tume ya Utumishi wa Umma
  • Baraza la Mitihani
  • Tume ya ajira Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo

    Anuani: 2 Barabara ya Boma, S.L.P 55, 57382 NAMTUMBO

    Simu ya Mezani: 0252675008

    Simu ya Mkononi: 0767519181

    Barua Pepe: ded@namtumbodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki©2021Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo. Haki zote Zimehifadhiwa.