• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Complaints |
    • Gms |
Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu ya Halmashauri
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji/Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi, Maliasili na Utalii
      • Mipango, Uchumi na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Utumishi na Utawala
      • Maji
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi na Zimamoto
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA)
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • TASAF
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Fursa za Kilimo
    • Fursa za ufugaji
    • Fursa za Madini
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Huduma za Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Mheshimiwa Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokalika
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Taarifa
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma/Vyombo Mbalimbali vya Habari
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali

Wananchi Namtumbo walalamikia ukubwa wa jimbo la Namtumbo

Tarehe ya Kuweka: October 10th, 2023

WANANCHI NAMTUMBO WALALAMIKIA  UKUBWA WA JIMBO LA  NAMTUMBO



.

Wakizungumza  kwa masikitiko makubwa kwenye ziara ya Mbunge wa Jimbo hilo Vitta Rashidi Kawawa ,wananchi hao walisema jimbo la Namtumbo ni kubwa sana hali inayomfanya mbunge wao kufanya kazi kubwa ya kuzungukia jimbo hilo na kuwahudumia wananchi .

Ajira ghaibu Kuluchi mwananchi wa kijiji cha Magazini alimwambia mbunge wa jimbo la Namtumbo kuwa Jimbo la Namtumbo ni kubwa mno hali inayomfanya mbunge wao kuzungukia jimbo hilo na kuzungumza na wananchi kwa kutumia muda mrefu ukifananisha na ukubwa wa  majimbo mengine.

Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi wilaya ya Namtumbo Zuberi Lihuwi pamoja na kukiri kuwa Jimbo la Namtumbo ni kubwa alifafanua kuwa vikao vya kisheria vya maendeleo vya wilaya( DCC) pamoja na vikao vya kisheria vya maendeleo vya mkoa vimepitisha maombi hayo ya kuomba jimbo la Namtumbo kugawika na kuwa majimbo mawili.

Hata hivyo Lihuwi alifafanua vigezo vya kugawa jimbo ni kuwa na idadi kubwa ya watu pamoja na ukubwa wa eneo la wilaya yetu hivyo akadai sensa ya mwaka 2022 itasaidia mamlaka kuona malalamiko ya wananchi ya Namtumbo yanaukweli kiasi gani alisema Lihuwi.

Pamoja na Hayo Lihuwi aliwataka wananchi kuwa watulivu  kuhusu  ujenzi wa  barabara  ya mtwarapachani –Nalasi mpaka Tunduru  kwa kuwa barabara hiyo ipo kwenye ilani ya Chama cha Mapinduzi  ya 2020-2025 baada ya wananchi hao kudai barabara hiyo kuchelewa kujengwa.

Diwani wa kata ya Magazini Grace Kapinga alimpongeza mbunge wa jimbo la Namtumbo kwa ushirikiano wake anaowapatia wananchi wa kata yake kwa kuhakikisha kero ya muda mrefu ya wananchi wa kata ya magazini kuhusu huduma ya afya inatatuliwa kwa kujengwa kituo cha afya na kupatikana kwa vifaa tiba ili kuanzishwa kwa kituo hicho.

Kapinga pamoja na mambo mengine alimwambia mbunge kuwa wananchi wa kata yake wanafuraha sana kuhusu kupatiwa milioni 500 za kujenga kituo cha afya cha magazini pamoja na kupatiwa vifaa tiba vyenye thamani ya shilingi milioni 65.

Mganga Mkuu wa wilaya ya Namtumbo Aaron Hyera alimshukuru Mbunge wa Namtumbo kwa kuipambania wilaya ya Namtumbo ili kuondoa changamoto za huduma za afya  zinazowakabili wananchi wa wilaya ya Namtumbo kuhakikisha fedha zinapatikana za ujenzi wa vituo vya afya na zahanati wilayani Namtumbo.

Vitta Rashid Kawawa Mbunge wa jimbo la  Namtumbo aliwashukuru wananchi waliofika katika kuhudhuria mkutano wake na kudai kuwa serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Dkt Samia Suluhu Hassan  inatekeleza mambo kwa vitendo.

Kawawa  aliwaambia wananchi kuwa serikali ya awamu ya sita imetoa fedha nyingi katika utekelezaji wa miradi mbalimbali wilayani Namtumbo haijawahi kutokea kuwepo kwa utekelezaji wa miradi yenye fedha nyingi kama serikali hii inayoongozwa na DKT Samia Suluhu Hassan.

Hata hivyo Kawawa aliwahatarisha wananchi kuwa kuna wapotoshaji wanapita na kuwadanganya wananchi kuwa barabara ya Mtwarapachani –Nalasi mpaka Tunduru fedha zake zimehamishwa na kupelekwa kujenga barabara ya Lumecha-Kitanda mpaka kidatu mkoa wa Morogoro na kuwataka wananchi hao kuachana na wapotoshaji hao.

Aidha Kawawa alifafanua kuwa Serikali imeweka vipaumbele katika ujenzi wa barabara Nchini ,vipaumbele hivyo vinasema barabara zinazounganisha nchi na nchi kipaumbele cha kwanza ,lakini barabara zinazounganisha mkoa na mkoa kipaumbele cha pili na barabara zinazounganisha wilaya ni kipaumbele cha tatu.

Barabara inayosemwa kuwa zimehamishwa hela na kwenda barabara ya Lumecha mpaka kidatu mkoa wa morogoro hiyo ni barabara ya kuunganisha mkoa na mkoa na ya mtwarapachani –Nalasi mpaka Tunduru barabara hiyo ni ya kuunganisha wilaya kwa wilaya na  bado haijapatiwa hela na kuwataka wananchi kuwa na subira wakati serikali inatafuta hela ya kujenga barabara hiyo badala ya kupotoshwa alisema Kawawa.

Wilaya ya Namtumbo ina ukubwa wa kilomita za mraba 20,375.1 ni wilaya kubwa kuliko wilaya zingine za mkoa wa Ruvuma ikifuatiwa na wilaya ya Tunduru yenye ukubwa wa kilomita za mraba 18,000 hali inayowafanya wananchi wa wilaya hiyo kuomba jimbo ili kumwezesha mbunge kuwafikia wananchi wa jimbo lake kwa wakati na kuwahudumia.

Mwisho.

 

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA 2025 KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA NAMTUMBO January 18, 2025
  • MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI KATIKA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA NAMTUMBO MWAKA 2025 January 12, 2025
  • Ona zote

Habari Mpya

  • DC NGOLLO MALENYA AWAFARIJI WAHANGA WA RADI KATIKA KATA YA LUSEWA WILAYA YA NAMTUMBO

    February 21, 2025
  • WANANCHI NAMTUMBO WAMSHUKURU RAIS SAMIA

    January 06, 2025
  • MATREKTA aliyogawa Rais Samia yawanufaisha wananchi wa Wilaya ya Namtumbo, katika kuongeza Uzalishaji kwenye kilimo cha Kisiasa.

    January 06, 2025
  • Sukrani kwa Mhe.Rais wa wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan

    January 05, 2025
  • Ona zote

Video

HOTUBA YA WAZIRI WA TAMISEMI
Video

Kurasa za Haraka

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Halmashauri ya Songea
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Nyasa
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru

Tovuti Mashuhuri

  • TAMISEMI
  • Ikulu ya Tanzania
  • Tume ya Utumishi wa Umma
  • Baraza la Mitihani
  • Tume ya ajira Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo

    Anuani: 2 Barabara ya Boma, S.L.P 55, 57382 NAMTUMBO

    Simu ya Mezani: 0252675008

    Simu ya Mkononi: 0767519181

    Barua Pepe: ded@namtumbodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki©2021Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo. Haki zote Zimehifadhiwa.